• Wasiliana nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mafia District Council
Mafia District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais , Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mafia

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Ardhi, Mipango miji na Maliasili
      • Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
        • Kitengo cha Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Kilimo na Ushirika
      • Ujenzi na Zima Mmoto
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango na Takwimu
    • Vitengo
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ufugaji Nyuki
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Tehama
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
      • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Huduma za jamii
      • Maadili
      • Fedha, Utawala, na Mipango
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Kujua Sheria
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za Ofisi au Kitaifa
      • YOUTUBE
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

CHUO CHA VETA MAFIA CHATOA WAHITIMU KWA MARA YA KWANZA TANGU KUANZISHWA

Posted on: November 23rd, 2025

Ili kuhakikisha elimu inaboreshwa nchini, Serikali iliweka jitihada ya kujenga vyuo vya VETA 25 vya wilaya ili kuwawezesha vijana kuwa na uwezo wa kutumia maarifa wanayopata kujiajiri pamoja na kuongeza ufanisi kwa wale wanaopata ajira rasmi sehemu mbalimbali. 

Miongoni mwa wilaya zilizonufaika na hatua hiyo ni wilaya ya Mafia ambapo matunda yameanza kuonekana baada ya chuo cha VETA wilayani hapo kutoa wahitimu 51 tangu kuanzishwa kwa chuo hicho mwaka 2024. 

Akizungumza wakati wa mahafali ya kwanza ya chuo hicho, Mkuu wa Wilaya ya Mafia Mhe. Aziza Mangosongo amewataka wazazi kulipa kipaumbele suala la elimu kwa kuhakikisha watoto wanapata elimu katika ngazi tofauti kwa kuwapeleka shule pamoja na vyuo ili kuwajengea msingi mzuri katika maisha yao. 

Mhe. Mangosongo amewasisitiza wazazi kuwaandikisha vijana chuoni hapo mara tu nafasi za masomo zinapotangazwa maana Serikali imejizatiti kutoa elimu bora kwa kuboresha miundombinu pamoja na kuweka samani na vifaa ili vijana wapate ujuzi utakaowasaidia kuchangia maendeleo ya Taifa. 

Aidha, amewasisitiza wanafunzi wanaoendelea na masomo chuoni hapo kutodanganyika na vishawishi vyovyote na badala yake wazingatie masomo na lengo lililowapeleka chuoni ili waongeze ujuzi utakaosaidia kuwakomboa kiuchumi na kuchangia maendeleo nchini. 

Kwa upande wake, Mkuu wa Chuo cha VETA Mafia Ndugu Salim Jumbe ameishukuru Serikali kwa kuendelea kuinua sekta ya elimu nchini kwa kuanzisha vyuo vya VETA ili kuwasaidia vijana, pia ametoa wito kwa vijana kujiunga na kozi zinazotolewa chuoni hapo za muda mrefu na muda mfupi maana Serikali imeweka gharama nafuu kuhakikisha wananchi wengi wananufaika.


Matangazo

  • MWALIKO WA KUHUDHURIA BARAZA LA KWANZA LA MADIWANI November 29, 2025
  • Tazama zote

Habari za hivi punde

  • CHUO CHA VETA MAFIA CHATOA WAHITIMU KWA MARA YA KWANZA TANGU KUANZISHWA

    November 23, 2025
  • WITO WATOLEWA KWA WADAU KUSHIRIKIANA NA SERIKALI KUBORESHA ELIMU

    November 21, 2025
  • JITIHADA ZAIDI ZAHITAJIKA KUBORESHA MASUALA YA LISHE WILAYANI MAFIA

    November 14, 2025
  • WANUFAIKA WAASWA KUTUMIA MIKOPO YA ASILIMIA 10 KWA MALENGO YALIYOKUSUDIWA

    November 13, 2025
  • Tazama zote

Video

USIKOSE KUWA SEHEMU YA TUKIO HILI MUHIMU KIHISTORIA
Tazama Video zaidi

Viungo vya haraka

  • Home
  • Photo Gallery
  • FAQ
  • Tourism
  • Investment
  • MATOKEO YA STD VII 2022

Viungo vinavyohusiana

  • OR- TAMISEMI
  • OR- Menejimenti Utumishi wa Umma
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Pwani
  • Sekretarieti ya ajira katika Utumishi wa Umma
  • Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi
  • Wizara ya Fedha na Mipango

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Free Visitor&Stat Counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kilindoni-Bomani Street

    Anuani ya posta: 85

    Simu: 0232010199

    Simu ya mkononi:

    Baruapepe: ded.mafia@pwani.go.tz / ded@mafiadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Katazo
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma namba 1
    • YOUTUBE

Copyright ©2017 Mafia District Council . All rights reserved.