Kamati ya Siasa ya Chama cha Mapinduzi ( CCM) Wilaya ya Mafia yaipongeza Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini ( RUWASA) kwa usimamizi na utekelezaji mzuri wa miradi ya maji.
Pongezi hizo zimetolewa Machi 26, 2025 na Katibu wa Siasa, Mafunzo na Uenezi wa CCM Wilaya ya Mafia, Issa Kombo wakati wa ziara ya kutembelea na kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa wilayani humo.
" Katika taasisi ambayo Chama cha Mapinduzi inatuheshimisha, ni RUWASA" alieleza Ndugu Kombo akionesha kuridhishwa na utekelezaji wa miradi iliyopo wilayani Mafia ikiwemo mradi wa maji wa kijiji cha Kifinge pamoja na mradi wa maji katika eneo la Magemani, kata ya Kilindoni.
Mradi mwigine uliokaguliwa ni pamoja na zahanati ya Kibada iliyopo kata ya Baleni ambapo Kamati imesisitiza kuwepo kwa mipango endelevu katika miradi pamoja na ushirikishwaji ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora.
Kilindoni-Bomani Street
Anuani ya posta: 85
Simu: 0232010199
Simu ya mkononi:
Baruapepe: ded.mafia@pwani.go.tz / ded@mafiadc.go.tz
Copyright ©2017 Mafia District Council . All rights reserved.