Maafisa Kilimo Wilayani Mafia wamepatiwa mafunzo juu ya ubora wa korosho kutoka kwa bodi ya korosho Tanzania. Mafunzo hayo yalitolewa kwa maafisa ugani na maafisa Kilimo waliopo Wilayani makao makuu.
Mafunzo hayo yatawasaidia maafisa Kilimo kwenda kutoa Elimu kwa wakulima namna ya kupata korosho bora , kuanzia utunzaji wa Shamba , namna ya kuvuna na kizihifadhi ili zisiharibu ubora. Bodi ya korosho walieleza kuwa korosho Bora ni Ile inayokomaa na kudondoka yenyewe chini na inatakiwa eneo la mti wa korosho kuwa safi kwani ubora wa korosho huharibiwa na unyevu/ maji kupitia bibo ambalo ndiyo linalolisha korosho huwa bichi.
Ukusanyaji wa korosho unatakiwa kufanyika kila siku na ukichelewa ndani ya siku tatu (03), bibo na korosho vitenganishwe mapema kwani bibo huendelea kuilisha korosho inayoweza kupelekea korosho kupata vimelea vinavyopunguza ubora wa korosho.
Uanikaji wa korosho ni kati ya siku 3-4 na zigeuzwe pande zote zipate jua na zikauke vizuri. Korosho zikikauka zitengwe zenye ujazo mkubwa na nzuri zisizoathiriwa na kuvu na kuhifadhiwa kwenye magunia maalum ya katani yaliyothibitishwa na TBS.
Pia walishauriwa ili kulinda ubora wa korosho ziuzwe ndani ya mwaka mmoja na wakulima wasisahau kubakisha korosho kwa ajili familia zao kwani zinasaidia sana macho pia waliongeza kuwa Afisa Ugani ambaye Kata yake itatoa korosho bora zaidi katika mkoa wa Pwani atapatiwa Zawadi na bodi ya korosho.
Kilindoni-Bomani Street
Anuani ya posta: 85
Simu: 0232010199
Simu ya mkononi:
Baruapepe: ded.mafia@pwani.go.tz / ded@mafiadc.go.tz
Copyright ©2017 Mafia District Council . All rights reserved.