• Wasiliana nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mafia District Council
Mafia District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais , Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mafia

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Ardhi, Mipango miji na Maliasili
      • Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
        • Kitengo cha Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Kilimo na Ushirika
      • Ujenzi na Zima Mmoto
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango na Takwimu
    • Vitengo
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ufugaji Nyuki
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Tehama
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
      • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Huduma za jamii
      • Maadili
      • Fedha, Utawala, na Mipango
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Kujua Sheria
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za Ofisi au Kitaifa
      • YOUTUBE
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

MAFIA YAADHIMISHA KILELE CHA WIKI YA CHANJO

Posted on: April 30th, 2025

Halmashauri ya Wilaya ya Mafia imeadhimisha kilele cha wiki ya chanjo kiwilaya leo Aprili 30, 2025 kwa kutoa elimu kwa kina mama na wasichana. 

Mkuu wa Wilaya ya Mafia na mgeni rasmi katika maadhimisho hayo Mhe. Aziza Mangosongo amewataka wazazi kuwa makini kwa kuwapeleka watoto katika vituo vya kutolea huduma ya afya kupata chanjo ili kuzuia magonjwa ya mlipuko kama Polio na Surua Rubella.

Aidha, amewataka wazazi na walezi kushirikiana katika malezi ya watoto hasa kwa kina baba kuhudhuria kliniki na wenza wao bila kuwaachia majukumu hayo wanawake peke yao.

Akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa zoezi la uchanjaji, Mratibu wa Chanjo wa Wilaya Ndugu Hussein Rajab ameeleza kuwa Wilaya inatarajia kufika asilimia 96 ya kiwango cha uchanjaji kutoka asilimia 90, hatua ambayo inachangiwa na uanzishwaji wa huduma ya chanjo katika zahanati mpya ya Kibada iliyopo kata ya Baleni.

Ndugu Rajab ameeleza kuwa baadhi ya changamoto zilizopo ni pamoja na baadhi ya wanajamii kuwa na imani potofu kuhusu chanjo zitolewazo kwa watoto, na kuwataka wazazi kuachana na imani hizo ili wajitokeze kupata elimu ya chanjo na kukamilisha dozi kama inavyotakiwa.

Baadhi ya wazazi waliowapeleka watoto wao kupata chanjo wametoa wito kwa wazazi wenzao kuzingatia umuhimu wa chanjo kwa watoto wao kama inavyoshauriwa." Nawahamasisha kina mama wenzangu kuwaleta watoto kupata chanjo na kufuata ushauri na maelekezo ya daktari kwa kuzingatia umuhimu wa chanjo hizo" alisema Khadija Issa, mkazi wa kata ya Kilindoni.

Vituo 26 kati ya vituo 28 vilivyopo wilayani Mafia vinatoa huduma ya chanjo vituoni na kupitia huduma za mkoba katika ngazi ya jamii.

Kauli mbiu ya maadhimisho ya chanjo inasema kwamba " Chanjo ni Kinga, Tuungane Kuwezesha Walengwa Wote Wapate Chanjo".


Matangazo

  • TANGAZO LA KUFUNGULIWA KWA DIRISHA LA UTOAJI WA MIKOPO May 02, 2025
  • Tazama zote

Habari za hivi punde

  • WADAU WADHAMIRIA KUONGEZA THAMANI ZAO LA MWANI

    April 30, 2025
  • MAFIA YAADHIMISHA KILELE CHA WIKI YA CHANJO

    April 30, 2025
  • MAFUNZO YA MFUMO WA UKAGUZI YATOLEWA KWA WAKUU WA DIVISHENI NA VITENGO

    April 29, 2025
  • MRADI WA MAJIKO BANIFU WATAMBULISHWA MAFIA

    April 28, 2025
  • Tazama zote

Video

MWENGE WA UHURU WAPONGEZA VIWANGO VYA BARABARA YA MSUFINI
Tazama Video zaidi

Viungo vya haraka

  • Home
  • Photo Gallery
  • FAQ
  • Tourism
  • Investment
  • MATOKEO YA STD VII 2022

Viungo vinavyohusiana

  • OR- TAMISEMI
  • OR- Menejimenti Utumishi wa Umma
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Pwani
  • Sekretarieti ya ajira katika Utumishi wa Umma
  • Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi
  • Wizara ya Fedha na Mipango

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Free Visitor&Stat Counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kilindoni-Bomani Street

    Anuani ya posta: 85

    Simu: 0232010199

    Simu ya mkononi:

    Baruapepe: ded.mafia@pwani.go.tz / ded@mafiadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Katazo
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma namba 1
    • YOUTUBE

Copyright ©2017 Mafia District Council . All rights reserved.