• Wasiliana nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mafia District Council
Mafia District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais , Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mafia

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Ardhi, Mipango miji na Maliasili
      • Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
        • Kitengo cha Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Kilimo na Ushirika
      • Ujenzi na Zima Mmoto
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango na Takwimu
    • Vitengo
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ufugaji Nyuki
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Tehama
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
      • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Huduma za jamii
      • Maadili
      • Fedha, Utawala, na Mipango
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Kujua Sheria
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za Ofisi au Kitaifa
      • YOUTUBE
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

MARUFUKU UTOAJI WA AJIRA KWA WATOTO; AONYA DC MANGOSONGO

Posted on: June 16th, 2025

Mkuu wa Wilayaya Mafia Mhe. Aziza Mangosongo ametoa onyo kwa wananchi wanaojihusisha na vitendo vya ukatili kufuatia vitendo vya uvunjifu wa sheria dhidi ya watoto ikiwemo ajira za utotoni pamoja na unyanyasaji.

Akizungumza wakati wa maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Afrika leo Juni 16, 2025, Mhe. Mangosongo amewataka wananchi kuzingatia sheria zinazomlinda mtoto dhidi ya unyanyasaji wowote pamoja na kuwanyima watoto haki za msingi ikiwemo elimu kwa kutoa ajira za utotoni.

" Kwa upande wa Mafia, ajira nyingi za utotoni tunazipata kwa wavuvi, na hiyo ni kinyume cha sheria na taratibu na ni kumkosesha mtoto haki ya kusoma na kutimiza ndoto zake. Niwatake wamiliki wa mitumbwi, mabaharia na manahodha kutowachukua watoto kwenda nao kwenye uvuvi" alisema Mhe. Mangosongo akisisitiza kuwa Serikali haitoruhusu vitendo hivyo vishamiri bila kuchukua hatua stahiki.

Mhe. Mangosongo ameeleza kuwa vitendo vya unyanyasaji kwa watoto ni jambo ambalo hatolifumbia macho kwa kuhakikisha kuwa wahalifu wanachukuliwa hatua ili kukomesha ukatili kwa watoto hasa ikizingatiwa kuwa vitendo vya ukatili wilayani Mafia bado vimeendelea kukithiri kwa muda mrefu.

Kwa kipindi cha Januari hadi Desemba 2024, jumla ya matukio 463 ya ukatili yaliripotiwa katika dawati la polisi na ustawi wa jamii wilayani ambapo matukio yanayoongoza kuripotiwa ni ukatili wa kijinsia kwa kuwa na matukio 245, ukatili wa kimwili matukio 111, ukatili wa kutelekezwa matukio 63 pamoja na ukatili wa kingono matukio 54 yakiwemo matukio ya mimba za utotoni.

Aidha, ametoa wito kwa wazazi kushirikiana na walimu na viongozi mbalimbali katika jamii kutokomeza tabia ya utoro kwa wanafunzi ambapo matukio mengi ya kihalifu hufanywa na wanafunzi watoro kwa kujihusisha na vitendo vya uvunjifu wa sheria kama utumiaji wa dawa za kulevya, na kujihusisha na mapenzi katika umri mdogo, jambo ambalo hupelekea mimba za utotoni.

Kuanzia Januari mwaka huu 2025 hadi sasa, mimba za utotoni tisa (9) zimeripotiwa wilayani Mafia, hivyo wananchi wameendelea kupewa wito kuripoti vitendo vya ukatili katika jamii kwani Serikali imeanzisha dawati la jinsia na watoto ili kurahisisha utoaji wa huduma na kunusuru watoto dhidi ya vitendo viovu ambapo vituo vya kipolisi 420 kote nchini vinatoa huduma kwa wananchi.

Kauli mbiu ya Siku ya Mtoto wa Afrika kwa mwaka huu 2025 ni " Haki za Watoto, Tulipotoka, Tulipo na Tuendako".

Matangazo

  • TANGAZO: MATOKEO YA USAILI KWA KAZI ZA MKATABA KWA NAFASI ZA UDEREVA NA UHUDUMU WA OFISI May 20, 2025
  • Tazama zote

Habari za hivi punde

  • MARUFUKU UTOAJI WA AJIRA KWA WATOTO; AONYA DC MANGOSONGO

    June 16, 2025
  • WANANCHI WAASWA KUJALI AFYA ZAO KUEPUKA MADHARA MAKUBWA YANAYOWEZA KUTOKEA

    June 14, 2025
  • DC MANGOSONGO AWAPOKEA WASHINDI WA UMISSETA NGAZI YA MKOA

    June 06, 2025
  • WANANCHI WILAYANI MAFIA WAASWA KUTUNZA MAZINGIRA KUKABILIANA NA MABADILIKO YA TABIANCHI

    May 31, 2025
  • Tazama zote

Video

MWENGE WA UHURU WAPONGEZA VIWANGO VYA BARABARA YA MSUFINI
Tazama Video zaidi

Viungo vya haraka

  • Home
  • Photo Gallery
  • FAQ
  • Tourism
  • Investment
  • MATOKEO YA STD VII 2022

Viungo vinavyohusiana

  • OR- TAMISEMI
  • OR- Menejimenti Utumishi wa Umma
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Pwani
  • Sekretarieti ya ajira katika Utumishi wa Umma
  • Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi
  • Wizara ya Fedha na Mipango

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Free Visitor&Stat Counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kilindoni-Bomani Street

    Anuani ya posta: 85

    Simu: 0232010199

    Simu ya mkononi:

    Baruapepe: ded.mafia@pwani.go.tz / ded@mafiadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Katazo
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma namba 1
    • YOUTUBE

Copyright ©2017 Mafia District Council . All rights reserved.