Mwenge wa Uhuru umezindua barabara ya kiwango cha lami yenye urefu wa Mita 950 iliyopo kijiji cha Kilindoni katika kitongoji cha Msufini.
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa barabara hiyo yenye thamani ya Shilingi Bilioni 1.3, Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Ndugu Ismail Ussi, amepongeza usimamizi wa mradi huo na kutoa wito kwa wananchi kuendelea kuitunza barabara hiyo ili iwanufaishe kwa muda mrefu zaidi.
" Mwenge wa uhuru umeridhishwa na mradi huu wa barabara ambayo imejengwa kwa kisasa, ubora na umadhubuti wa viwango vyote. Niwaombe ndugu wananchi na wakazi wa eneo hili tuendelee kuitunza barabara hii maana ni maendeleo ambayo Serikali inayosimamiwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan inalenga katika kuhudumia wananchi wake" alieleza
Kwa upande wake, Diwani wa kata ya Kilindoni ambaye ni Mwenyekiti wa Halmashauri Mhe. Juma Salum ameipongeza Serikali kwa kuendelea kuwajali wananchi kwa kuboresha miundombinu.
" Wakati Mhe. Rais anaingia madarakani, hatukuwa na hii barabara, tulikuwa na barabara moja tu yenye KM 14 wilayani Mafia, leo hii tumepata barabara ya kwanza ya mtaa kwenye Halmashauri yetu, na huu mfano wa barabara ni mmoja tu, kuna mengi yamefanyika katika kipindi cha miaka minne katika maeneo mbalimbali " alieleza Mhe. Salum.
Kilindoni-Bomani Street
Anuani ya posta: 85
Simu: 0232010199
Simu ya mkononi:
Baruapepe: ded.mafia@pwani.go.tz / ded@mafiadc.go.tz
Copyright ©2017 Mafia District Council . All rights reserved.