Mwenge wa Uhuru umekimbizwa leo Aprili 07, 2025 wilayani Mafia baada ya kukabidhiwa kutoka Wilaya ya Kibiti ambapo mkuu wa Wilaya hiyo Kanali Joseph Kolombo aliukabidhi rasmi kwa Mkuu wa Wilaya ya Mafia Mhe. Aziza Mangosongo.
Miradi 11 imekaguliwa, miradi mitatu imezinduliwa, na mradi mmoja umewekewa jiwe la msingi na kufanya jumla ya miradi 15 yenye thamani ya Bilioni 2.8 kutembelewa na Mwenge wa Uhuru kwa kukimbizwa kwa umbali wa KM 64.9 ndani ya wilaya ya Mafia.
Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Ismail Ussi ameonesha kuridhishwa kwa kupongeza usimamizi na utekelezaji wa miradi wilayani Mafia huku akisisitiza kuendeleza uzalendo kwa kufanya kazi kwa bidii pamoja na kutoa wito kwa wananchi kuitunza miradi hiyo ili iwe ya manufaa kwa sasa na baadaye.
" Mwenge wa Uhuru umeridhishwa na utekelezaji wa miradi wilayani hapa, muendelee kutunza miradi hii maana inatekelezwa kwa fedha nyingi, kwa kufanya hivyo tutakuwa tunayaishi mazuri yanayofanywa na Serikali chini ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan" alieleza Ussi.
Mwenge wa Uhuru unatarajiwa kukabidhiwa kesho Aprili 8, 2025 wilayani Bagamoyo.
Kilindoni-Bomani Street
Anuani ya posta: 85
Simu: 0232010199
Simu ya mkononi:
Baruapepe: ded.mafia@pwani.go.tz / ded@mafiadc.go.tz
Copyright ©2017 Mafia District Council . All rights reserved.