Benki ya Maendeleo ya Kilimo (TADB) imelenga kuitekeleza dhana ya uchumi wa buluu wilayani Mafia kupitia mradi wake wa miaka mitano ambao utawawezesha kiuchumi wakazi wa wilaya hiyo.
Mradi huo utanufaisha vikundi nane vya kijasiriamali kwa kuwakabidhi mkopo wa boti nane zitakazotumika katika shughuli za kilimo cha mwani pamoja na uvuvi.
"Mkopo huu utawapa fursa wajasiriamali kutekeleza shughuli zao na watapata kipindi cha neema kwa miezi mitatu ya mwanzo kwa kutofanya marejesho. Ni malengo ya serikali kuona kuwa boti zitatumika kwa shughuli zilizokusudiwa" alisema Richard Sembindu, Afisa Biashara kutoka Benki ya Maendeleo ya Kilimo kanda ya Mashariki.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mafia, Mwl. Kassim Ndumbo, ameipongeza serikali kupitia wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa kufika Mafia na kwa lengo la kuimarisha na kukuza uchumi kwa wilaya na wakazi wake kiujumla.
Kilindoni-Bomani Street
Anuani ya posta: 85
Simu: 0232010199
Simu ya mkononi:
Baruapepe: ded.mafia@pwani.go.tz / ded@mafiadc.go.tz
Copyright ©2017 Mafia District Council . All rights reserved.