• Wasiliana nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mafia District Council
Mafia District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais , Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mafia

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Ardhi, Mipango miji na Maliasili
      • Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
        • Kitengo cha Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Kilimo na Ushirika
      • Ujenzi na Zima Mmoto
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango na Takwimu
    • Vitengo
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ufugaji Nyuki
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Tehama
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
      • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Huduma za jamii
      • Maadili
      • Fedha, Utawala, na Mipango
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Kujua Sheria
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za Ofisi au Kitaifa
      • YOUTUBE
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

uwekezaji

Utangulizi.

Wilaya ya Mafia ni Miongoni mwa Wilaya sita (6) katika Mkoa wa Pwani. Wilaya zingine ni pamoja na Bagamoyo, Kibaha, Kisarawe, Mkuranga na Rufiji. Kijiografia Wilaya ya Mafia ni mkusanyiko wa Visiwa vinane kwenye Bahari ya Hindi km 195 kusini mwa Jiji la Dar es Salaam. Visiwa hivyo ni Mafia (kisiwa kikuu), Jibondo, Mbarakuni, Shungimbili, Nyororo, Juani, Bwejuu na Chole. Visiwa vya Mbarakuni, Shungimbili na Nyororo ni vya makazi ya muda tu ya wavuvi. Kisiwa cha mafia kinapatikana kati ya longitudi 39°E – 40°E na latitude 7.38oS.


ENEO NA MIPAKA YA WILAYA.

Wilaya ya Mafia ina Eneo la kilometa za mraba 972, kati ya hizo Kilometa za mraba 407 ni nchi kavu na 565 ni eneo la maji ya Bahari ya Hindi ambayo ni sawa na asilimia 58.73 ya eneo lote. Upande wa kaskazini, Mafia imepakana na Wilaya za Mkuranga na Kibiti, kusini Magharibi na wilaya ya Kilwa na upande wa kusini Mashariki imepakana na Bahari ya Hindi.

IDADI YA WATU.

Katika Sensa ya watu na makazi ya mwaka 2022, Wilaya ilikuwa na watu 66,180 wanaume 33,220 na wanawake 32,960 ikiwa na ongezeko la asilimia 3.6 kwa mwaka na wastani wa watu 4 kwa kaya.

HALI YA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI.

Wilaya ya Mafia ina jumla ya viwanda 20 kati ya hivyo, kimoja (1) ni kikubwa, vinne (4) vya kati na kumi na tano (15) vidogo. Viwanda hivi vinajumuisha viwanda  vya uchakataji wa mazao ya bahari,viwanda vya mafuta ya nazi,ufyatuaji tofali,utengenezaji wa samani,uzalishaji wa barafu na ushonaji. Aidha, Wilaya ya Mafia kuna hoteli za kitalii nane (8) na nyumba za kulala wageni (Lodging Houses) kumi na nane (18) na nyumba za kulala wageni (Guest Houses) kumi na nne (14). Pia wilaya ya Mafia ina vituo vya kuogelea (Diving Center) tatu (3). Hadi sasa Wilaya ya Mafia ina jumla ya Maduka ya nusu jumla(sub-wholesaler) tisa (9) na rejareja na biashara zinginezo zipatazo mia sita sitini na nane (668). Sambamba na uwepo wa biashara hizi, wilaya ya Mafia tuna uhitaji mkubwa kwenye fursa mbalimbali za uwekezaji katika maeneo tofauti kama ifuatavyo:

FURSA ZA KIUCHUMI ZILIZOPO.

 i. Bahari 

  •  Uvuvi. Uwepo wa eneo la bahari ya Hindi ambalo linachukua kilometa za mraba 565 kunapelekea fursa za kuwekeza kwenye viwanda vya usindikaji mazao yatokanayo na bahari, Ujenzi wa miundombinu ya uvuvi na zana bora za kisasa kwa ajili ya uvuvi endelevu.
  •  Usafirishaji wa baharini. Wilaya ya Mafia inafikika kwa kutumia njia kuu mbili ambazo ni usafiri wa anga na usafiri wa majini. Hata hivyo, kwa hivi sasa hakuna usafiri wa uhakika wa maji kuvutia wawekezaji kuja kuwekeza Mafia kwani njia hii bado haijawa rafiki kwa wageni au watalii wanaopendelea kutumia usafiri wa njia ya Bahari.

Kilimo cha Mwani. Miaka ya hivi karibuni, kilimo cha mwani kimekuwa ni shughuli muhimu sana kiuchumi ikisaidia kupunguza kasi ya uvunaji wa samaki na mazao mengine ya bahari. Kwa wilaya ya Mafia, zao la Mwani limekuwa na manufaa kwa kuongeza kipato na ajira kwa kina mama kwa kuwa hawakuwa na fursa ya kujishughulisha na shughuli nyingine zaidi ya uvuvi. Kwa mwaka 2022/23 jumla ya tani 690 za mwani zilivunwa. Fursa nyinginezo katika kilimo cha Mwani ni pamoja na kuchakata na kuongeza thamani ya zao la mwani, kutengeneza bidhaaa mbalimbali zitokanazo na mwani.

                     

Vivutio vya Utalii.

 Mazalia ya Samaki matumbawe na Michezo ya Uzamiaji (Diving and Snorkling) Idadi kubwa ya vivutio vilivyopo baharini kunaifanya Mafia kuwa sehemu ya utalii wa kuzamia yenye hadhi ya kidunia (world class diving/snorkeling site). Kisiwa cha Mafia ni eneo muhimu la mazalia ya samaki linalokadiriwa kuwa na zaidi ya aina 400 za samaki. Pamoja na uwepo wa vivutio hivi vya baharini, bado idadi ya watalii wazamiaji imekua ni ndogo. Hivyo, juhudi za makusudi za kukitangaza kisiwa cha Mafia kama kituo cha michezo ya uzamiaji zitasaidia kuleta na kuongeza watalii wa ndani na nje.


Matangazo

  • TANGAZO: NAFASI ZA KAZI ZA MUDA; AFISA MIFUGO MSAIDIZI July 14, 2025
  • Tazama zote

Habari za hivi punde

  • CAG ASISITIZA USIMAMIZI MZURI WA MAPATO

    June 19, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YAKAGUA MIRADI YA ELIMU NA SOKO

    June 19, 2025
  • KLINIKI YA ARDHI YAIFIKIA MAFIA

    June 18, 2025
  • VETA YATOA MAFUNZO KWA MAMA LISHE ZAIDI YA 200 WA KATA YA KILINDONI

    June 17, 2025
  • Tazama zote

Video

Kisiwa cha Mafia ndani ya SGR
Tazama Video zaidi

Viungo vya haraka

  • Home
  • Photo Gallery
  • FAQ
  • Tourism
  • Investment
  • MATOKEO YA STD VII 2022

Viungo vinavyohusiana

  • OR- TAMISEMI
  • OR- Menejimenti Utumishi wa Umma
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Pwani
  • Sekretarieti ya ajira katika Utumishi wa Umma
  • Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi
  • Wizara ya Fedha na Mipango

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Free Visitor&Stat Counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kilindoni-Bomani Street

    Anuani ya posta: 85

    Simu: 0232010199

    Simu ya mkononi:

    Baruapepe: ded.mafia@pwani.go.tz / ded@mafiadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Katazo
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma namba 1
    • YOUTUBE

Copyright ©2017 Mafia District Council . All rights reserved.