• Wasiliana nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mafia District Council
Mafia District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais , Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mafia

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Ardhi, Mipango miji na Maliasili
      • Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
        • Kitengo cha Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Kilimo na Ushirika
      • Ujenzi na Zima Mmoto
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango na Takwimu
    • Vitengo
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ufugaji Nyuki
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Tehama
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
      • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Huduma za jamii
      • Maadili
      • Fedha, Utawala, na Mipango
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Kujua Sheria
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za Ofisi au Kitaifa
      • YOUTUBE
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

CAG ASISITIZA USIMAMIZI MZURI WA MAPATO

Posted on: June 19th, 2025

Halmashauri ya Wilaya ya Mafia imetakiwa kuongeza nguvu katika usimamizi wa mapato na kuendelea kutenga fedha za kukamilisha miradi iliyosimama kwa muda mrefu.

Akitoa maagizo hayo Juni 19, 2025 kwa niaba ya Katibu Tawala wa Mkoa wakati wa Mkutano Maalum wa Baraza la Madiwani lililolenga kujadili taarifa za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali ( CAG), Katibu Tawala Msaidizi Mkoa wa Pwani Sehemu ya Mipango na Uratibu Bi. Edna Katalaiya, ameeleza kuwa usimamizi mzuri wa ukusanyaji wa mapato utasaidia kuongeza pato la Halmashauri ambalo litatumika katika shughuli mbalimbali za kimaendeleo ili wananchi wapate huduma iliyokusudiwa.

" Tunaelekezwa kwenye miongozo ya uandaaji wa bajeti za Serikali kwamba, kabla hatujaanza miradi mipya, tuhakikishe miradi viporo imekamilika na itoe huduma kwa wananchi" alisisitiza Bi. Katalaiya.

Pamoja na mambo mengine, Halmashauri imetakiwa kuhakikisha inabuni vyanzo vipya vya mapato pamoja na kusimamia vyema vyanzo vilivyopo kwa kuongeza wigo wa ukusanyaji na kuanzisha miradi mikakati itakayosaidia kuongeza mapato na kukuza ajira kwa vijana.

Katika hatua nyingine, Bi. Katalaiya amewasisitiza wakuu wa Idara na Vitengo kusimamia matumizi mazuri ya mfumo wa kujibu hoja na kuondokana na matumizi ya karatasi katika kujibu hoja mbalimbali na kuwasisitiza kudumisha umoja katika utendaji kazi na kuhakikisha hawazalishi hoja mpya.

Hadi kufikia Juni 15, 2025 Halmashauri ya Wilaya ya Mafia imefanikiwa kufunga hoja 16 kati ya hoja 34 za mwaka wa fedha 2023/ 2024.

Aidha, ameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Mafia kwa kupata Hati safi kwa miaka mitano mfululizo kuanzia mwaka 2020 hadi sasa, pamoja na kukusanya asilimia 96 ya mapato mpaka kufikia tarehe 17 Juni, 2025 hali ambayo inatoa mwelekeo mzuri wa kufikia lengo la kukusanya asilimia 100 na zaidi. 

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Halmashauri Mhe. Juma Salum ameipongeza Serikali kwa kuleta mabadiliko makubwa ndani ya miaka mitano, hatua ambayo Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameendelea kuchochea uwekezaji katika kisiwa cha Mafia hasa katika utalii , pamoja na kuleta fedha za utekelezaji wa miradi ya elimu, afya, maji, umeme na barabara.


Matangazo

  • TANGAZO: NAFASI ZA KAZI ZA MUDA; UCHAGUZI MKUU July 02, 2025
  • Tazama zote

Habari za hivi punde

  • CAG ASISITIZA USIMAMIZI MZURI WA MAPATO

    June 19, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YAKAGUA MIRADI YA ELIMU NA SOKO

    June 19, 2025
  • KLINIKI YA ARDHI YAIFIKIA MAFIA

    June 18, 2025
  • VETA YATOA MAFUNZO KWA MAMA LISHE ZAIDI YA 200 WA KATA YA KILINDONI

    June 17, 2025
  • Tazama zote

Video

Kisiwa cha Mafia ndani ya SGR
Tazama Video zaidi

Viungo vya haraka

  • Home
  • Photo Gallery
  • FAQ
  • Tourism
  • Investment
  • MATOKEO YA STD VII 2022

Viungo vinavyohusiana

  • OR- TAMISEMI
  • OR- Menejimenti Utumishi wa Umma
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Pwani
  • Sekretarieti ya ajira katika Utumishi wa Umma
  • Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi
  • Wizara ya Fedha na Mipango

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Free Visitor&Stat Counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kilindoni-Bomani Street

    Anuani ya posta: 85

    Simu: 0232010199

    Simu ya mkononi:

    Baruapepe: ded.mafia@pwani.go.tz / ded@mafiadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Katazo
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma namba 1
    • YOUTUBE

Copyright ©2017 Mafia District Council . All rights reserved.