Mkuu wa Wilaya ya Mafia Mhe. Aziza Mangosongo ameitaka Halmashauri kuhakikisha kuwa inaweka mazingira bora ya uwekezaji katika sekta mbalimbali ikiwemo utalii, viwanda na biashara kupitia fursa mbalimbali zipatikqnazo kisiwani Mafia.
Mhe. Mangosongo ameyasema hayo leo Januari 15, 2026 wakati wa kikao cha Kamati ya Ushauri ya Wilaya ( DCC) kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri uliopo Chicco kilichohusisha viongozi wa Serikali wilayani Mafia, viongozi wa vyama vya siasa, viongozi wa dini, watumishi kutoka taasisi mbalimbali za Kiserikali na wananchi.
Mhe. Mangosongo ameeleza kuwa ni muhimu wataalam wa Halmashauri kwa kushirikiana na taasisi zinazojihusisha na utalii pamoja na wadau, kuhakikisha kuwa Mafia inapiga hatua kiuchumi kwa kutanua wigo wa uwekezaji.


" Tuone namna ya kuvutia wawekezaji, nimeona kwenye bajeti kuwa mmetenga fedha kwa ajili ya kubuni maeneo ya uwekezaji, basi tuwe ' serious' na kufanya kweli, pia tuyatangaze ili wawekezaji wajue wanaanzia wapi" alieleza Mhe. Mangosongo mara baada ya uwasilishaji wa bajeti kutoka Halmashauri pamoja na taasisi nyingine.
Katika hatua nyingine ya kuhakikisha maendeleo yanapatikana kwa kasi wilayani, Mhe. Mangosongo ameitaka Halmashauri kuweka mkazo katika ukusanyaji wa mapato na kubuni vyanzo vipya vya mapato vitakavyosaidia kuijenga Mafia kiuchumi.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mafia Mhe. Gulam Mohammed ametoa wito kwa wananchi kutoa ushirikiano wao katika sekta zote wakisaidiana na wataalam kutoka Halmashauri na taasisi mbalimbali ili kuiinua Mafia kiuchumi.
Aidha, amesisitiza umuhimu wa kulinda maadili katika jamii akiwaomba viongozi wa dini kuendelea kutoa elimu kwa wananchi ili kuendelea kulinda mila na deaturi pamoja na kudumisha amani na kufanya kazi kwa bidii kuijenga Mafia na Taifa kwa ujumla.


Kilindoni-Bomani Street
Anuani ya posta: 85
Simu: 0232010199
Simu ya mkononi:
Baruapepe: ded.mafia@pwani.go.tz / ded@mafiadc.go.tz
Copyright ©2017 Mafia District Council . All rights reserved.