• Wasiliana nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mafia District Council
Mafia District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais , Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mafia

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Ardhi, Mipango miji na Maliasili
      • Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
        • Kitengo cha Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Kilimo na Ushirika
      • Ujenzi na Zima Mmoto
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango na Takwimu
    • Vitengo
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ufugaji Nyuki
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Tehama
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
      • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Huduma za jamii
      • Maadili
      • Fedha, Utawala, na Mipango
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Kujua Sheria
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za Ofisi au Kitaifa
      • YOUTUBE
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

JITIHADA ZIONGEZWE KUTOKOMEZA MALARIA

Posted on: June 17th, 2025

Mkuu wa Wilaya ya Mafia Mhe. Aziza Mangosongo ametoa wito kwa jamii kuendelea kuunga mkono jitihada za Serikali za kutokomeza ugonjwa wa malaria kwa kufuata ushauri unaotolewa na wataalam wa afya pamoja na kuzingatia usafi katika mazingira yanayowazunguka.

Wito huo umetolewa leo Juni 17, 2025 wakati wa uzinduzi wa Afua ya Viuadudu ( Biorlavicide) iliyofanyika eneo la Kigamboni lililopo kata ya Kilindoni ambapo Mhe. Mangosongo aliambatana na Idara ya Afya kutembelea eneo hilo kwa lengo la kupulizia dawa katika bwawa ambalo limekuwa chanzo kikubwa cha mazalia ya mbu.

" Nitoe wito kwa wataalam wa afya kuendelea kutoa elimu kwa jamii juu ya namna ya kupambana na malaria, vilevile niwaombe wazazi kuwa makini kwa kuhakikisha watoto hawachezi maeneo haya hatarishi na kuhakikisha wanatumia chandarua kuzuia kuenea kwa malaria pamoja na kwenda vituo vya kutoa huduma ya afya pindi wanapopata changamoto za afya, badala ya kutumia dawa bila kufika vituoni" alieleza Mhe. Mangosongo.

Kwa upande wake, Afisa Afya wa Wilaya ya Mafia Ndugu Othman Masanga ameeleza kuwa Idara ya Afya inaendelea kutoa elimu kuhusu afya, hasa kupambana na malaria kwa jamii kutumia vyandarua na kusafisha mazingira kuzuia mazalia ya mbu ili Wilaya iweze kutimiza lengo la Serikali la kutokomeza kabisa malaria ( Zero Malaria) ifikapo mwaka 2030.

Halmashauri ya Wilaya ya Mafia imeendelea na afua za kupambana na kukabiliana na ugonjwa wa malaria na kupelekea kupungua kwa maambukizi toka asilimia 22.9 kwa robo ya Oktoba hadi Desemba 2024 mpaka asilimia 18.5 kwa robo ya Januari hadi Machi 2025.

Katika hatua nyingine ya kuhakikisha ugonjwa wa malaria unatokomezwa, Mhe. Mangosongo ameielekeza Wakala ya Barabara Tanzania ( TANROADS) kutengeneza mitaro itakayosaidia kuondosha maji ambayo yamekuwa yakituama katika eneo hilo kwa muda mrefu na kuwa kero kwa wakazi wanaozunguka bwawa hilo.

" Niwape pole wakazi wanaozunguka eneo hili lakini niwahakikishie kwamba Serikali yetu chini ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan inawajali na itaendelea kuchukua hatua nzuri kutatua kero zenu. Naielekeza TANROADS kuja kuangalia na kuona namna ya kutengeneza mtaro, hata kwa kutenga fedha za dharura ili wananchi waondokane na kero hii" alisema Mhe. Mangosongo.

Wilaya ya Mafia ina jumla ya mabwawa 59 ambayo yamekuwa yakizalisha mbu kwa wingi na kupelekea kuenea kwa maambukizi ya malaria, hata hivyo, Halmashauri ya Wilaya ya Mafia imepokea lita 3000 za viuadudu zenye thamani ya Shilingi Milioni 39.6 kutoka Wizara ya Afya kupitia Mpango wa Taifa wa kudhibiti malaria.

Wananchi wa Mafia, hasa wakazi wa maeneo ambayo yamekuwa yakizalisha mbu kwa wingi, wametoa shukrani zao kwa Serikali na kuiomba iboreshe miundombinu ya barabara kwa kuweka mitaro ili maji yasituame katika makazi yao.



Matangazo

  • TANGAZO: NAFASI ZA KAZI ZA MUDA; UCHAGUZI MKUU July 02, 2025
  • Tazama zote

Habari za hivi punde

  • VETA YATOA MAFUNZO KWA MAMA LISHE ZAIDI YA 200 WA KATA YA KILINDONI

    June 17, 2025
  • JITIHADA ZIONGEZWE KUTOKOMEZA MALARIA

    June 17, 2025
  • MARUFUKU UTOAJI WA AJIRA KWA WATOTO; AONYA DC MANGOSONGO

    June 16, 2025
  • WANANCHI WAASWA KUJALI AFYA ZAO KUEPUKA MADHARA MAKUBWA YANAYOWEZA KUTOKEA

    June 14, 2025
  • Tazama zote

Video

MWENGE WA UHURU WAPONGEZA VIWANGO VYA BARABARA YA MSUFINI
Tazama Video zaidi

Viungo vya haraka

  • Home
  • Photo Gallery
  • FAQ
  • Tourism
  • Investment
  • MATOKEO YA STD VII 2022

Viungo vinavyohusiana

  • OR- TAMISEMI
  • OR- Menejimenti Utumishi wa Umma
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Pwani
  • Sekretarieti ya ajira katika Utumishi wa Umma
  • Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi
  • Wizara ya Fedha na Mipango

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Free Visitor&Stat Counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kilindoni-Bomani Street

    Anuani ya posta: 85

    Simu: 0232010199

    Simu ya mkononi:

    Baruapepe: ded.mafia@pwani.go.tz / ded@mafiadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Katazo
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma namba 1
    • YOUTUBE

Copyright ©2017 Mafia District Council . All rights reserved.