• Wasiliana nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mafia District Council
Mafia District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais , Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mafia

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Ardhi, Mipango miji na Maliasili
      • Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
        • Kitengo cha Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Kilimo na Ushirika
      • Ujenzi na Zima Mmoto
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango na Takwimu
    • Vitengo
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ufugaji Nyuki
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Tehama
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
      • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Huduma za jamii
      • Maadili
      • Fedha, Utawala, na Mipango
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Kujua Sheria
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za Ofisi au Kitaifa
      • YOUTUBE
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

KAMATI YA FEDHA KUTEMBELEA MIRADI

Posted on: May 3rd, 2021

Kwa kipindi cha robo ya tatu(Januari- Machi) mwaka fedha 2020/2021 tarehe 29/04/2021 Kamati ya Fedha, utawala na Mipango ikiongozwa na Mwenyekiti wa Halmashauri Mh. Juma Salum Ally ilitembelea miradi mitano ya Halmashauri iliyopo Tarafa ya Kaskazini kama ifuatavyo;-

1.         Zahanati ya Kijiji cha Gonge.

Zahanati iko hatua ya umaliziaji kwa kupaka rangi na kuingiza umeme, kujenga placenta pit, kichomea taka na nyumba ya watumishi. Kamati ilikuta kazi ya umaliziaji inaendelea. Kamati iliridhishwa na hatua iliyofikiwa na ilishauri menejimenti iweke mikakati ya kuhakikisha zahanati inapokamilika ipate mahitaji kama samani, vifaa tiba na watumishi angalau wachache kwa kuanzia.

2.         Zahanati ya Kijiji cha Kifinge.

Kazi ya umaliziaji inaendelea aidha bado placenta pit, kichomea taka na nyumba ya watumishi havijajengwa. Wajumbe walishauri mifuko ya saruji iliyoazimishwa shule ya msingi Kifinge irejeshwe ili kukamilisha ujenzi uliosalia ikiwemo nyumba ya watumishi. Wajumbe walishauri sehemu ya mbele ya jengo la zahanati kimwagwe kifusi kudhibiti adha ya maji na tope. Mheshimiwa diwani kata ya Baleni aliwathibitishia wajumbe kuwa suala la kifusi liko ndani ya uwezo wao watakamilisha. Kamati iliridhishwa na hatua iliyofikiwa na ilishauri menejimenti iweke mikakati ya kuhakikisha zahanati inapokamilika ipate mahitaji kama samani, vifaa tiba na watumishi angalau wachache kwa kuanzia.

3.         Kituo cha Afya Kirongwe

Wajumbe walisema kuwa gharama zilizotumika kujenga kituo ni kubwa lakini huduma zinazotolewa hazishawishi wagonjwa kutibiwa hapo. Sababu ni upungufu wa watumishi, vifaa tiba na miundombinu mingine. Walishauri Halmashauri itafute namna ya kuhakikisha Kituo kinapata mahitaji yote muhimu ili kitoe huduma bora za tiba.

Pia suala la usafi lilionekana kuwa kero maana kituo kimejaa nyasi zisizofyekwa. Hivyo kamati ilishauri Halmashauri ya Kijiji cha Kirongwe iweke utaratibu wa kufanya usafi kwa kushirikiana na kamati ya usimamizi wa kituo hicho.

 

4.         Zahanati ya Kijiji cha Jimbo.

Pamoja na mwonekano wa jengo kuwa imara, wajumbe walijionea mpasuko wa ukuta uliosababishwa na asili ya udongo wa eneo hilo. Hivyo walitaka kujua utaratibu ukoje kuhakikisha zahanati inafanyiwa marekebisho na inafanya kazi. Akifafanua juu ya hatua zilizopo Kaimu Afisa Mipango (W) alisema tayari milioni 50 zimeshatengwa kwa ajili ya kukamilisha kazi zote ili jengo lifanye kazi. Kaimu mhandisi Ujenzi aliongezea kuwa milioni 50 zikiingia zitatosha kuhakikisha jengo linakamilika na kuanza kutumika.  

Kamati ilimwelekeza Mkurugenzi Mtendaji (W) kuhakikisha kuwa ndani ya mwezi wa tano 2021 fedha iwe imepelekwa kukamilisha ujenzi wa jengo hilo.

5.         Eneo la Mwalo na Mnada katika Kijiji cha Bweni.

Wajumbe walikagua eneo la mwalo lililopendekezwa kujengwa mnada wa samaki katika kijiji cha Bweni. Kaimu mwandisi ujenzi aliwataarifu wajumbe kuwa kwa kuanzia zikipatikana milioni 5 kazi itafanyika na mnada utaanza. Wajumbe waliridhia na kumwagiza Mkurugenzi Mtendaji (W) kuendelea na ujenzi wa banda la mnada ili kudhibiti utoroshwaji wa mapato na kuongeza mapato kwa wananchi, kijiji na Halmashauri.

Mwenyekiti wa Halmashauri alihitimisha kwa kuwashukuru wajumbe na kupongeza jitihada zinazoendelea kufanyika katika kutekeleza miradi ya maendeleo ili kuchochea ongezeko la mapato na huduma bora kwa jamii ya watanzania.

 

Matangazo

  • TANGAZO LA KUONGEZWA MUDA WA KULIPIA VIWANJA May 20, 2025
  • Tazama zote

Habari za hivi punde

  • WITO WATOLEWA KWA WATOTO WA KIKE KUPENDA MASOMO YA SAYANSI

    May 17, 2025
  • MAFIA KUUNGANISHWA NA UMEME WA GRIDI YA TAIFA

    May 16, 2025
  • WANANCHI WAASWA KUJITOKEZA KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 16, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI LARIDHIA KUANZISHWA KWA MRADI WA UONGEZAJI THAMANI ZAO LA DAGAA

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

MWENGE WA UHURU WAPONGEZA VIWANGO VYA BARABARA YA MSUFINI
Tazama Video zaidi

Viungo vya haraka

  • Home
  • Photo Gallery
  • FAQ
  • Tourism
  • Investment
  • MATOKEO YA STD VII 2022

Viungo vinavyohusiana

  • OR- TAMISEMI
  • OR- Menejimenti Utumishi wa Umma
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Pwani
  • Sekretarieti ya ajira katika Utumishi wa Umma
  • Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi
  • Wizara ya Fedha na Mipango

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Free Visitor&Stat Counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kilindoni-Bomani Street

    Anuani ya posta: 85

    Simu: 0232010199

    Simu ya mkononi:

    Baruapepe: ded.mafia@pwani.go.tz / ded@mafiadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Katazo
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma namba 1
    • YOUTUBE

Copyright ©2017 Mafia District Council . All rights reserved.