Nimeridhishwa na hatua iliyofikiwa ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo inayotekelezwa katika Halmashauri ya Wilaya Mafia, Katibu Tawala Pwani aliyasema haya alipokuwa katika ziara tarehe 04/11/2022 alipotembelea miradi mbalimbali ikiwemo ujenzi wa shule ya sekondari Jibondo iliyopo kijiji cha Jibondo ambayo kijiografia kijiji cha Jibondo ni kisiwa , pamoja na changamoto za upelekaji wa vifaa vya ujenzi , hatua iliyofikiwa katika ujenzi ni nzuri
Mradi wa ujenzi wa kituo cha afya Kiegeani ambacho kwa sasa ujenzi wa majengo umekamilika, zikiwemo jengo la wagonjwa wa nje (OPD), nyumba mbili kwa nne za watumishi wa kituo , kichomea taka, sehemu ya kufulia nguo , miundombinu ya maji na umeme isipokuwa majengo yaliyoongezeka ambayo ujenzi unaendelea na uwekaji wa miundombinu
Mradi wa jengo la ofisi ambalo lipo katika hatua ya umaliziaji kazi ya upakaji rangi, na umaliziaji wa miundombinu , kuweka madirisha , blandaring zinaendelea
Ujenzi wa majengo ya dharura (EMD) na wagonjwa mahututi (ICU) majengo yapo hatua za umaliziaji ambapo alielekeza kasoro zilizobainika zirekebishwe
Mradi wa ujenzi wa shule ya Msingi Kigamboni ambapo ujenzi wa madarasa, Jengo la utawala na nyumba za walimu unaendelea
Mwisho alitembelea ujenzi wa shule mpya ya sekondari Ndagoni na kujionea mradi unavyoondelea na changamoto kubwa ilikuwa ni upungufu wa vifaa ikiwemo sementi.
Mwisho alihitimisha kwa kusema kuwa uongozwe umakini zaidi katika hatua za umaliziaji (finishing) ili majengo yaonekane nadhifu , imara nanubora wake ujidhihirishe. Pia aliwashukuru wananchi wa Mafia ka kiridhirishwa kwao na uongozi wa serikali ya awamu sita chini ya Mh. Rais Samia Suluhu Hassan na kuahidi atazifikisha salamu na shukrani zao.
Kilindoni-Bomani Street
Anuani ya posta: 85
Simu: 0232010199
Simu ya mkononi:
Baruapepe: ded.mafia@pwani.go.tz / ded@mafiadc.go.tz
Copyright ©2017 Mafia District Council . All rights reserved.