• Wasiliana nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mafia District Council
Mafia District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais , Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mafia

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Ardhi, Mipango miji na Maliasili
      • Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
        • Kitengo cha Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Kilimo na Ushirika
      • Ujenzi na Zima Mmoto
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango na Takwimu
    • Vitengo
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ufugaji Nyuki
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Tehama
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
      • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Huduma za jamii
      • Maadili
      • Fedha, Utawala, na Mipango
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Kujua Sheria
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za Ofisi au Kitaifa
      • YOUTUBE
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

KIKAO CHA BARAZA LA MADIWANI KUPITIA NA KUJADILI TAARIFA YA MDHIBITI NA MKAGUZI WA HESABU ZA SERIKALI (CAG) MWAKA 2019/2020.

Posted on: June 14th, 2021

Kikao cha Baraza la madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Mafia cha kupitia na kujadili taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali (CAG) kilifanyika siku ya tarehe 14/06/2021 katika ukumbi wa Magereza.

 Katika kikao hicho alishiriki pia Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhe. Abubakar Kunenge , Katibu Tawala  Mkoa wa Pwani Mhandisi Mwanasha Tumbo pamoja na mwakilishi kutoka ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa Serikali mkoa wa Pwani.

Mhe. Abubakari Kunenge Mkuu wa Mkoa wa Pwani aliipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Mafia kwa kupata hati safi pia aliwataka kufunga hoja za ukaguzi kabla hazijafika kwenye hatua ya kutakiwa kujieleza ili kuepuka kuzalisha hoja zaidi.

Mkuu wa Mkoa amewataka watumishi kufuata taratibu, kanuni na kuheshimu sheria za utumishi wa umma na kuwasilisha nyaraka za matumizi yote ya Fedha zinazohitajika wakati wa ukaguzi ili kuepuka kuzalisha Hoja.

Nukuu "Sitopenda kuona hoja zinaongezeka na kujirudia kwa mwaka ujao" alisema Kunenge

Pia ameitaka Halmashauri kubuni vyanzo vipya vya mapato, kusimamia ukusanyaji wa mapato na pia kudhibiti matumizi.

Alitoa rai pia kwa Viongozi wote wa Kisiasa na Kitaalamu Wilayani kushirikiana katika kutekeleza majukumu yao na kuwaasa wafanya maamuzi kupokea ushauri wa kitaalam ili wafanye maamuzi sahihi.

Alieleza kuwa amekuja kufanya kazi Mkoa wa Pwani na kuwataka wataalamu wote Mkoani hapo kuandaa taarifa yenye Fursa zote muhimu katika sekta zilizopo Mkoani hapo ikiwemo vyanzo vya Mapato, Huduma za Kijamii, Viwanda Kilimo, Biashara, Utalii, Uvivu ili kupata hali ilivyo kwa sasa na kuainisha maeneo yote yanayohitaji maboresho.

Kupitia Taarifa hiyo inayooenesha fursa mbalimbali katakuwa na Siasa nzuri ya kiuchumi ya kutumia kidogo kupata kingi na kwa kuvifanyia kazi vipaumbele hivyo muhimu kutaleta maendeleo ya haraka ya Wilaya na Mkoa kwa ujumla.

Pia aliongezea kwa kusema kuwa kuwa ili kuleta maendeleo ya haraka katika wilaya ya Mafia ni lazima viongozi na wafanyakazi kuondokana na dhana ya kuwa '' Mafia ni eneo la pembezoni lililotengwa na kutothaminiwa bali kuanza kuinadi upya Wilaya ya Mafia''.

Akieleza kuhusu changamoto ya uhaba wa watumishi, Taa kwenye Kiwanja cha Ndege, Tozo kwa mizigo na magari mara mbili kwenye Bandari ya Nyamisati na Kilindoni mafia amesema ameyachukua na atayafanyia kazi.

Pamoja na mambo mengine Mhe. Kunenge alipokea taarifa ya Wilaya na pia alipata fursa ya kuzungumza na Baraza la Madiwani na Kutembelea Kiwanda kikubwa cha kuchakata Samaki cha TANPESCA Ltd.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUONGEZWA MUDA WA KULIPIA VIWANJA May 20, 2025
  • Tazama zote

Habari za hivi punde

  • KIJIJI CHA DONGO KUPATA KITUO CHA AFYA

    May 23, 2025
  • COWOFO MAFIA YATEMBELEA WAGONJWA HOSPITALI YA WILAYA

    May 21, 2025
  • WITO WATOLEWA KWA WATOTO WA KIKE KUPENDA MASOMO YA SAYANSI

    May 17, 2025
  • MAFIA KUUNGANISHWA NA UMEME WA GRIDI YA TAIFA

    May 16, 2025
  • Tazama zote

Video

MWENGE WA UHURU WAPONGEZA VIWANGO VYA BARABARA YA MSUFINI
Tazama Video zaidi

Viungo vya haraka

  • Home
  • Photo Gallery
  • FAQ
  • Tourism
  • Investment
  • MATOKEO YA STD VII 2022

Viungo vinavyohusiana

  • OR- TAMISEMI
  • OR- Menejimenti Utumishi wa Umma
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Pwani
  • Sekretarieti ya ajira katika Utumishi wa Umma
  • Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi
  • Wizara ya Fedha na Mipango

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Free Visitor&Stat Counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kilindoni-Bomani Street

    Anuani ya posta: 85

    Simu: 0232010199

    Simu ya mkononi:

    Baruapepe: ded.mafia@pwani.go.tz / ded@mafiadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Katazo
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma namba 1
    • YOUTUBE

Copyright ©2017 Mafia District Council . All rights reserved.