• Wasiliana nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mafia District Council
Mafia District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais , Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mafia

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Ardhi, Mipango miji na Maliasili
      • Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
        • Kitengo cha Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Kilimo na Ushirika
      • Ujenzi na Zima Mmoto
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango na Takwimu
    • Vitengo
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ufugaji Nyuki
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Tehama
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
      • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Huduma za jamii
      • Maadili
      • Fedha, Utawala, na Mipango
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Kujua Sheria
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za Ofisi au Kitaifa
      • YOUTUBE
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

KITUO CHA AFYA KIRONGWE CHAFANYA UPASUAJI WA KWANZA KWA KINA MAMA WAJAWAZITO

Posted on: February 18th, 2025

Kituo cha Afya cha Kirongwe kimezindua rasmi huduma ya upasuaji kwa kina mama, leo Februari 18, 2025  ambapo upasuaji uliofanyika kwa mama mjamzito umekamilika salama. 

Kituo hicho kilichoanza kutoa huduma za afya tangu mwaka 2020 hakikuwahi kuwa na huduma ya upasuaji kutokana na sababu mbalimbali ambazo  ziliwalazimu wananchi kufuata huduma hiyo katika Hospitali ya Wialya. 

"Kwa kuanzisha huduma hii hapa, tumewasogezea wananchi huduma karibu zaidi. Tunashukuru Serikali kwa kutuongezea rasilimali watu wakiwemo madaktari na wahudumu wengine, pamoja na kutuboreshea miundombinu kama majengo, jenereta, na vifaa mbalimbali ambavyo mwanzo vilikuwa sababu ya kutokuwa ha huduma hii" ameeleza Kaimu Mganga Mkuu wa Wilaya, Ndg. Omary Mvoulana. 

Kwa upande wake, Diwani wa kata ya Kirongwe Mhe. Said Msabaha ameishukuru Serikali kwa kuendelea kujali wananchi hasa katika sekta ya afya. 

"Leo tumeanza kwa mama wa kwanza kujifungua salama, tunashukuru madaktari na wauguzi kwa hatua hii na tunapongeza jitihada za Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan za kuhakikisha huduma za afya, hasa kwa mama na mtoto, zinaboreshwa"  amesema Mhe. Msabaha. 

Akitoa shukrani zake baada ya kufanyika upasuaji, Kassim Hassan ambaye ni mume wa mzazi aliyejifungua mtoto wa kike, ameeleza hatua kubwa iliyofikiwa baada ya wananchi kupitia changamoto hapo awali. 

"Nashukuru mke wangu amejifungua salama, mwanzo nililazimika kumpeleka Hospitali ya Wilaya kujifungua mtoto wetu wa kwanza, lakini leo huduma hii ameipata hapa, tunamuomba Mungu awajalie viongozi wetu ili watuletee huduma kama hizi karibu yetu" alieleza Bw. Hassan. 

Hatua hii itasaidia kupunguza kero ya msongamano katika Hospitali ya Wilaya na kuleta mabadiliko chanya katika suala la afya ya mama na mtoto, ikiwemo kuokoa maisha yao pindi changamoto zinapotokea. 

" Tulikuwa tukisafiri kwa shida kufuata huduma Hospitali, ilikuwa shida kipindi cha masika na hali ya barabara si nzuri, baadhi ya wanawake walikuwa wakijifungua njiani, ila sasa tunaishukuru Serikali kwa maendeleo haya" alisema  Aisha Ahmad, mkazi wa kitongoji cha Shalaza.


Matangazo

  • TANGAZO LA KUONGEZWA MUDA WA KULIPIA VIWANJA May 20, 2025
  • Tazama zote

Habari za hivi punde

  • WITO WATOLEWA KWA WATOTO WA KIKE KUPENDA MASOMO YA SAYANSI

    May 17, 2025
  • MAFIA KUUNGANISHWA NA UMEME WA GRIDI YA TAIFA

    May 16, 2025
  • WANANCHI WAASWA KUJITOKEZA KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 16, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI LARIDHIA KUANZISHWA KWA MRADI WA UONGEZAJI THAMANI ZAO LA DAGAA

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

MWENGE WA UHURU WAPONGEZA VIWANGO VYA BARABARA YA MSUFINI
Tazama Video zaidi

Viungo vya haraka

  • Home
  • Photo Gallery
  • FAQ
  • Tourism
  • Investment
  • MATOKEO YA STD VII 2022

Viungo vinavyohusiana

  • OR- TAMISEMI
  • OR- Menejimenti Utumishi wa Umma
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Pwani
  • Sekretarieti ya ajira katika Utumishi wa Umma
  • Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi
  • Wizara ya Fedha na Mipango

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Free Visitor&Stat Counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kilindoni-Bomani Street

    Anuani ya posta: 85

    Simu: 0232010199

    Simu ya mkononi:

    Baruapepe: ded.mafia@pwani.go.tz / ded@mafiadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Katazo
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma namba 1
    • YOUTUBE

Copyright ©2017 Mafia District Council . All rights reserved.