• Wasiliana nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mafia District Council
Mafia District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais , Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mafia

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Ardhi, Mipango miji na Maliasili
      • Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
        • Kitengo cha Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Kilimo na Ushirika
      • Ujenzi na Zima Mmoto
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango na Takwimu
    • Vitengo
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ufugaji Nyuki
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Tehama
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
      • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Huduma za jamii
      • Maadili
      • Fedha, Utawala, na Mipango
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Kujua Sheria
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za Ofisi au Kitaifa
      • YOUTUBE
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

KOFIH YAKABIDHI JENGO LA MAMA NA MTOTO KWA HALMASHAURI

Posted on: August 28th, 2025

Taasisi ya KOFIH imekabidhi rasmi mradi wa jengo la mama na mtoto kwa Halmashauri ya Wilaya ya Mafia leo Agosti 28, 2025.

Makabidhiano hayo yaliyofanyika katika Hospitali ya Wilaya yameshuhudiwa na baadhi ya wataalam kutoka shirika hilo, Ofisi ya Mganga Mkuu wa Mkoa wa Pwani, wawakilishi kutoka Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Mafia, pamoja na wataalam wa Idara ya afya wakiongozwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri Ndugu Mussa Kitungi.

Akikabidhi mradi huo, Mwakilishi wa KOFIH nchini Tanzania Bw. Gyeongbae Seo amefurahishwa na juhudi za Serikali pamoja na uongozi wa Halmashauri kuhakikisha mradi unafikia hatua nzuri ambayo itawezesha wananchi kupata huduma bora.

" Tunapongeza jitihada za Halmashauri kuchangia pale ambapo tuliishia sisi na kuhakikisha inaonesha umiliki wa mradi huu. Jengo hili halitohudumia kina mama na watoto wakati huu yu, bali hata vizazi vijavyo" alieleza Bw. Seo.

Kwa upande wake, Mwakilishi wa Mganga Mkuu wa Mkoa wa Pwani Bi. Mercy Mtaita ameishukuru taasisi ya KOFIH kwa kuunga mkono juhudi za Serikali katika kuboresha afya ya mama na mtoto na kusisitiza juu ya utunzaji wa miundombinu iliyopo ili iweze kusaidia kina mama wengi wa Mafia na kupunguza rufaa nyingi za wananchi kwenda kutibiwa nje ya wilaya.Aidha, amewataka wahudumu wa afya kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi kwa kuzingatia miongozo iliyopo.

" Tutoe huduma kulingana na miongozo iliyowekwa tukiamini kwamba hata Mungu anatuona, tunaweza tusilipwe hapa duniani ila Mwenyezi Mungu akiangalia kazi tuliyofanya basi tutapewa thawabu zetu" alisisitiza.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mafia Ndugu Mussa Kitungi ameahidi kuwa Halmashauri itaitunza miundombinu iliyopo pamoja na kuhakikisha kuwa huduma inaimarishwa ili wananchi wapate kunufaika kama ilivyokusudiwa.

" Kutekelezwa kwa mradi huu kunadhihirisha ni kiasi gani Serikali inashirikiana vyema na taasisi mbalimbali za ndani na nje ya nchi, hivyo kukamilika kwa jengo hili kutaboresha huduma za afya wilayani" alieleza Ndugu Kitungi.

Taasisi ya KOFIH ilichangia kiasi cha Shilingi Milioni 270 katika utekelezaji wa mradi huo, huku Serikali ikitoa kiasi cha Shilingi Milioni 300 ili kuhakikisha jengo la mama na mtoto linakamilika.


Matangazo

  • TANGAZO: KUITWA KWENYE USAILI (UCHAGUZI MKUU 2025) October 05, 2025
  • Tazama zote

Habari za hivi punde

  • SIKU YA PAPA POTWE DUNIANI; JAMII YAASWA KUWAJIBIKA KUTUNZA MAZINGIRA

    August 30, 2025
  • KOFIH YAKABIDHI JENGO LA MAMA NA MTOTO KWA HALMASHAURI

    August 28, 2025
  • JAMII KUSHIRIKIANA NA WATAALAM KUREJESHA MSITU WA MLOLA

    August 26, 2025
  • WASIMAMIZI WA MIRADI WATAKIWA KUONGEZA UFANISI KATIKA UTEKELEZAJI

    August 22, 2025
  • Tazama zote

Video

USIKOSE KUWA SEHEMU YA TUKIO HILI MUHIMU KIHISTORIA
Tazama Video zaidi

Viungo vya haraka

  • Home
  • Photo Gallery
  • FAQ
  • Tourism
  • Investment
  • MATOKEO YA STD VII 2022

Viungo vinavyohusiana

  • OR- TAMISEMI
  • OR- Menejimenti Utumishi wa Umma
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Pwani
  • Sekretarieti ya ajira katika Utumishi wa Umma
  • Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi
  • Wizara ya Fedha na Mipango

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Free Visitor&Stat Counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kilindoni-Bomani Street

    Anuani ya posta: 85

    Simu: 0232010199

    Simu ya mkononi:

    Baruapepe: ded.mafia@pwani.go.tz / ded@mafiadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Katazo
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma namba 1
    • YOUTUBE

Copyright ©2017 Mafia District Council . All rights reserved.