• Wasiliana nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mafia District Council
Mafia District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais , Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mafia

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Ardhi, Mipango miji na Maliasili
      • Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
        • Kitengo cha Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Kilimo na Ushirika
      • Ujenzi na Zima Mmoto
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango na Takwimu
    • Vitengo
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ufugaji Nyuki
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Tehama
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
      • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Huduma za jamii
      • Maadili
      • Fedha, Utawala, na Mipango
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Kujua Sheria
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za Ofisi au Kitaifa
      • YOUTUBE
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

MAADHIMISHO YA WIKI LA JUMA YA ELIMU YA WATU WAZIMA

Posted on: September 26th, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Mafia, Mhe. Aziza Mangosongo akiwa ameambatana na kamati ya Usalama, uongozi wa Halmashauri pamoja na watumishi, amewaongoza wakazi wa Mafia katika maadhimisho ya Juma la Elimu ya Watu Wazima yaliyofanyika Septemba 26, 2024 katika Shule ya Sekondari ya Baleni.

Akizungumza katika maadhimisho hayo, Mhe. Mangosongo ameeleza namna Serikali ilivyojizatiti kuhakikisha elimu bora inapatikana kwa wananchi wa rika zote.

Aidha, amewataka wazazi kuwasimamia vyema watoto wao wawapo shuleni na nyumbani ili wazingatie elimu na kuepusha tabia za utoro pamoja na matendo yasiyofaa ambayo hupelekea ukatili wa kijinsia.

"Hatuwezi kukubali watoto wetu kufeli, Mhe. Rais Dkt Samia Suluhu Hassan analeta fedha nyingi ili wanafunzi wasome na wafaulu, natamani wazazi tuwalee watoto wetu kwa ubora kama sisi tulivyolelewa" alisema Mhe. Mangosongo.

Katika kuhakikisha elimu inaimarika, mwaka 2021 Serikali ilianzisha miradi mbalimbali ikiwemo SEQUIP na MEMKWA ambayo imewasaidia wasichana na wavulana walioacha shule kutokana na changamoto mbalimbali waweze kurejea kwenye masomo.

Mariam Juma ni mmoja wa wanafunzi wa kidato cha tano walionufaika na miradi hiyo kwa kumuwezesha kurudi shule baada ya kupata changamoto zilizopelekea kukatisha masomo yake.

" Nilianza elimu ya watu wazima mwaka 2022, nilihamasika kujiunga na elimu hii baada ya kumsikia Mhe. Rais akitutaka turudi shuleni" alisema Mariam. " Nilikata tamaa kabisa baada ya kukumbwa na changamoto, nilipata nafasi kuanza masomo na baada ya kufanya mtihani wa kidato cha nne nilifaulu na kuchaguliwa kujiunga kidato cha tano katika shule ya Sekondari Kitomondo, nawaomba mabinti wenzangu wasikate tamaa na warudi shuleni kutimiza malengo yao" aliongeza.

Kwa sasa, Halmashauri kupitia Idara ya Elimu Sekondari imeanzisha darasa la wanafunzi 19 wa elimu ya watu wazima na kuendelea kutoa hamasa kwa jamii ili kuhakikisha  wanatekeleza na kuunga mkono jitihada za Serikali za kuboresha elimu.

" Kupitia programu hii, nimeweza kugundua mambo mengi ambayo yanaweza kufanyiwa kazi na kutufikisha mahala ambapo Taifa, Mikoa na Halmashauri yanatarajiwa kufikiwa, ikiwemo kuhamasisha wanafunzi wote wa kike na wa kiume walioacha shule kurudi shule kuendelea na masomo na kutimiza ndoto zao" alisema Hawa Said, mratibu wa Kitengo cha Elimu ya Watu Wazima.

Maadhimisho ya Juma la Elimu ya Watu Wazima kwa mwaka 2024 yameongozwa na kauli mbiu isemayo " Ujumuishi katika Elimu Bila Ukomo kwa Ujuzi, Ustahimilivu, Amani na Maendeleo"

Matangazo

  • TANGAZO LA KUONGEZWA MUDA WA KULIPIA VIWANJA May 20, 2025
  • Tazama zote

Habari za hivi punde

  • WITO WATOLEWA KWA WATOTO WA KIKE KUPENDA MASOMO YA SAYANSI

    May 17, 2025
  • MAFIA KUUNGANISHWA NA UMEME WA GRIDI YA TAIFA

    May 16, 2025
  • WANANCHI WAASWA KUJITOKEZA KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 16, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI LARIDHIA KUANZISHWA KWA MRADI WA UONGEZAJI THAMANI ZAO LA DAGAA

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

MWENGE WA UHURU WAPONGEZA VIWANGO VYA BARABARA YA MSUFINI
Tazama Video zaidi

Viungo vya haraka

  • Home
  • Photo Gallery
  • FAQ
  • Tourism
  • Investment
  • MATOKEO YA STD VII 2022

Viungo vinavyohusiana

  • OR- TAMISEMI
  • OR- Menejimenti Utumishi wa Umma
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Pwani
  • Sekretarieti ya ajira katika Utumishi wa Umma
  • Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi
  • Wizara ya Fedha na Mipango

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Free Visitor&Stat Counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kilindoni-Bomani Street

    Anuani ya posta: 85

    Simu: 0232010199

    Simu ya mkononi:

    Baruapepe: ded.mafia@pwani.go.tz / ded@mafiadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Katazo
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma namba 1
    • YOUTUBE

Copyright ©2017 Mafia District Council . All rights reserved.