• Wasiliana nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mafia District Council
Mafia District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais , Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mafia

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Ardhi, Mipango miji na Maliasili
      • Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
        • Kitengo cha Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Kilimo na Ushirika
      • Ujenzi na Zima Mmoto
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango na Takwimu
    • Vitengo
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ufugaji Nyuki
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Tehama
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
      • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Huduma za jamii
      • Maadili
      • Fedha, Utawala, na Mipango
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Kujua Sheria
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za Ofisi au Kitaifa
      • YOUTUBE
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

MAFIA KUUNGANISHWA NA UMEME WA GRIDI YA TAIFA

Posted on: May 16th, 2025

Wananchi wa Wilaya ya Mafia wanatarajia kuondokana na changamoto ya upatikanaji wa umeme kupitia mradi mkubwa wa Gridi ya Taifa utakaosaidia upatikanaji wa umeme wa uhakika.

Mradi huo utahusisha kupitisha waya chini ya maji kwa urefu wa KM 70 na kina cha KM 1.5 kutoka Kisiju wilayani Mkuranga hadi Mafia, ambapo utapitishwa kwa urefu wa KM 6.5 kutoka fukweni, Tereni hadi Kichangachui.

"Tunaamini mradi huu utakuwa mwarobaini kwa tatizo la umeme wilayani Mafia, hivyo nawaomba tutoe ushirikiano kwa Serikali ili kufanikisha hatua hii" alisema Ndugu Jovinus Kyaruzi, Afisa Tawala wilaya ya Mafia katika mkutano uliofanyika eneo la Kigamboni, Mei 15, 2025.

Mradi huo unatarajiwa kupunguza gharama za uendeshaji kwa Serikali tofauti na hali ilivyo sasa ambapo Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) wilayani Mafia limekua likitumia gharama kubwa kununua mafuta ya kuendesha mitambo.

" Tunajaribu kupunguza gharama za uzalishaji wa umeme kwa kutumia gridi yaTaifa, maana tunatumia gharama kubwa kununua mafuta ya 'generator' hapa Mafia, gharama tutakazo okoa zitatumika kufanya shughuli nyingine za maendeleo " alisema mpimaji ardhi kutoka TANESCO, Ndugu Jafari Lindonde.

Akijibu swali lililoulizwa na mwananchi kuhusu ulipwaji wa fidia , Mthamini wa Wilaya ya Mafia Ndugu Philip Kubingwa ameeleza kuwa, kwa mujibu wa sheria za ardhi, miradi kama hii inaanza kwanza fidia na baadaye mradi kuendelea ili kuondoa sintofahamu kwa wananchi.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mafia Mhe. Juma Salum ameipongeza Serikali kupitia TANESCO kwa kuja na suluhisho la upatikanaji wa umeme wa uhakika kwa wakazi wa Mafia ili kurahisisha shughuli za kiuchumi na kijamii.

"Sisi maslahi yetu makubwa kwenu ni kuhakikisha anayestahili kulipwa fidia, analipwa . Tunawashukuru kwa kuupokea mradi huu ili na sisi wananchi wa Mafia tuunganishwe kwenye gridi ya Taifa na kuweza kufanya shughuli zetu za kiuchumi" alieleza Mhe. Salum.

Madi huu unahusisha upimaji shirikishi ambapo wananchi wanashirikishwa katika upimaji wa maeneo kabla ya kuanza kwa mradi.


Matangazo

  • TANGAZO: MATOKEO YA USAILI KWA KAZI ZA MKATABA KWA NAFASI ZA UDEREVA NA UHUDUMU WA OFISI May 20, 2025
  • Tazama zote

Habari za hivi punde

  • DC MANGOSONGO AWAPOKEA WASHINDI WA UMISSETA NGAZI YA MKOA

    June 06, 2025
  • WANANCHI WILAYANI MAFIA WAASWA KUTUNZA MAZINGIRA KUKABILIANA NA MABADILIKO YA TABIANCHI

    May 31, 2025
  • UKOSEFU WA ELIMU MIONGONI MWA VYANZO ZINAVYOSABABISHA VIFO VYA WAZAZI NA WATOTO

    May 29, 2025
  • MRADI WA KUTUNZA MSITU WA MLOLA WAWAZINDULIWA RASMI WILAYANI MAFIA

    May 26, 2025
  • Tazama zote

Video

MWENGE WA UHURU WAPONGEZA VIWANGO VYA BARABARA YA MSUFINI
Tazama Video zaidi

Viungo vya haraka

  • Home
  • Photo Gallery
  • FAQ
  • Tourism
  • Investment
  • MATOKEO YA STD VII 2022

Viungo vinavyohusiana

  • OR- TAMISEMI
  • OR- Menejimenti Utumishi wa Umma
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Pwani
  • Sekretarieti ya ajira katika Utumishi wa Umma
  • Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi
  • Wizara ya Fedha na Mipango

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Free Visitor&Stat Counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kilindoni-Bomani Street

    Anuani ya posta: 85

    Simu: 0232010199

    Simu ya mkononi:

    Baruapepe: ded.mafia@pwani.go.tz / ded@mafiadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Katazo
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma namba 1
    • YOUTUBE

Copyright ©2017 Mafia District Council . All rights reserved.