• Wasiliana nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mafia District Council
Mafia District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais , Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mafia

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Ardhi, Mipango miji na Maliasili
      • Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
        • Kitengo cha Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Kilimo na Ushirika
      • Ujenzi na Zima Mmoto
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango na Takwimu
    • Vitengo
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ufugaji Nyuki
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Tehama
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
      • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Huduma za jamii
      • Maadili
      • Fedha, Utawala, na Mipango
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Kujua Sheria
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za Ofisi au Kitaifa
      • YOUTUBE
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

MAFIA YAADHIMISHA SIKU YA USAFI DUNIANI

Posted on: September 21st, 2024

Wakazi wa Mafia wameadhimisha Siku ya Usafi Duniani kwa kusafisha fukwe katika kitongoji cha Tumbuju kilichopo kata ya Ndagoni pamoja na eneo la Soko Mjinga lililopo Kilindoni. 

Zoezi hilo limeongozwa na Kitengo cha Udhibiti wa Taka na Usafi wa Mazingira,serikali ya kata na kijiji, BMU,  kwa kushirikiana na vyombo vya usalama, kikundi cha Takataka Dampo kilichopo wilayani, na vikundi vya michezo (jogging).

Akitoa wito kwa wananchi kuzingatia usafi wa mazingira, Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Usimamizi wa Taka na Usafi wa Mazingira, Bwana Othman Masanga, amesisitiza umuhimu wa kufanya usafi kila siku kwa ajili ya kulinda afya na kutokomeza magonjwa ya mlipuko.

Kwa upande wao, wakazi wa kitongoji cha Tumbuju wameishukuru Serikali kupitia uongozi wa Halmashauri kwa kuhamasisha na kusimamia usafi, ambapo wameahidi kutoa ushirikiano ili kuboreaha mazingira yao ya biashara na makazi.

" Tumefurahi kuwa pamoja na viongozi wetu leo kwa kufanya usafi, tunaomba waendelee kuwawajibisha wasiozingatia usafi bila kuogopa ili fukwe zetu ziwe safi" alisema Mtoro Kimbau, mkazi wa Tumbuju.

Wananchi zaidi ya 80 wamejitokeza kufanya usafi katika fukwe, ambapo zaidi ya Tani moja ya taka zimekusanywa.

" Kwetu kama wadau wa mazingira, tumefurahi sana kwa ushirikiano mkubwa tuliopata na tunawaomba wananchi kuendelea kuongeza nguvu kutunza mazingira yetu" alisema Abdu Amrani, Mwenyekiti wa Kikundi cha Kijamii cha Takataka Dampo kinachojihusisha na Udhibiti wa taka wilayani Mafia.

Zoezi la usafi kwa kata ya Kilindoni lilihitimishwa na Ndugu Juma Salum mgeni rasmi ambaye ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mafia.

Siku ya Usafi Duniani kwa mwaka 2024 inaongozwa na kauli mbiu isemayo " Uhai Hauna Mbadala, Zingatia Usafi wa Mazingira".


Matangazo

  • TANGAZO LA KAZI YA UWAKALA WA KUKUSANYA MAPATO January 27, 2026
  • Tazama zote

Habari za hivi punde

  • WASIMAMIZI WA MIRADI WATAKIWA KUFUATA MIONGOZO YA SERIKALI KATIKA UTEKELEZAJI

    January 02, 2026
  • USHIRIKISHWAJI WA JAMII NI NGUZO KUBWA YA UTUNZAJI WA RASILIMALI ZA BAHARI

    December 30, 2025
  • NAMNA JAMII INAVYOSHIRIKI KATIKA UTUNZAJI WA MAZINGIRA

    December 28, 2025
  • JITIHADA ZA UHIFADHI ZALETA MATUMAINI KWA WAKAZI WA JIMBO

    December 18, 2025
  • Tazama zote

Video

WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA WAPEWA MSAADA WA VIFAA VYA SHULE
Tazama Video zaidi

Viungo vya haraka

  • Home
  • Photo Gallery
  • FAQ
  • Tourism
  • Investment
  • MATOKEO YA STD VII 2022

Viungo vinavyohusiana

  • OR- TAMISEMI
  • OR- Menejimenti Utumishi wa Umma
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Pwani
  • Sekretarieti ya ajira katika Utumishi wa Umma
  • Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi
  • Wizara ya Fedha na Mipango

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Free Visitor&Stat Counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kilindoni-Bomani Street

    Anuani ya posta: 85

    Simu: 0232010199

    Simu ya mkononi:

    Baruapepe: ded.mafia@pwani.go.tz / ded@mafiadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Katazo
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma namba 1
    • YOUTUBE

Copyright ©2017 Mafia District Council . All rights reserved.