Msimamizi wa Uchaguzi Halmashauri ya Wilaya ya Mafia, Ndugu Mussa Kitungi ametoa wito kwa vyama vya siasa wilayani kuhakikisha kuwa wananchi wanajitokeza kwa wingi kujiandikisha kupiga kura pamoja na kushiriki uchaguzi wa Serikali za Mitaa ifikapo Novemba 27, 2024.
Ndugu Kitungi ameyasema hayo ofisini kwake wakati akizungumza na viongozi wa Vyama vya siasa ambapo amesisitiza umuhimu wa ushirikishwaji wa wananchi katika kuhakikisha viongozi bora wanapatikana katika Halmashauri na Taifa kwa ujumla.
Miongoni mwa malengo ya kikao hicho, ni pamoja na Kupokea na kujadili vituo vya uchaguzi vitakavyotumika kuandikisha wapiga kura na kushiriki zoezi la kupiga kura.
Aliongeza kwa kuwaomba vyama vya siasa kuwa ni vyema kutumia nafasi ya kuendelea kuhamasisha wananchi kujitokeza kwa wingi kuanzia kwenye upataji wa elimu ya uchaguzi,kujiandikisha na kupiga kura.
Uandikishaji wa wapiga kura unatarajiwa kuanza ifikapo tarehe 11 hadi 20 Oktoba, 2024.
Mbali na kueleza hayo, Bw. Masasi alitoa shukrani za dhati kwa serikali kwa maelekezo na miongozo ya uchaguzi wa Serikali za mitaa kwani inaweka usawa na haki katika kushiriki zoezi hili la uchaguzi wa serikali za mitaa.
Kilindoni-Bomani Street
Anuani ya posta: 85
Simu: 0232010199
Simu ya mkononi:
Baruapepe: ded.mafia@pwani.go.tz / ded@mafiadc.go.tz
Copyright ©2017 Mafia District Council . All rights reserved.