• Wasiliana nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mafia District Council
Mafia District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais , Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mafia

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Ardhi, Mipango miji na Maliasili
      • Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
        • Kitengo cha Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Kilimo na Ushirika
      • Ujenzi na Zima Mmoto
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango na Takwimu
    • Vitengo
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ufugaji Nyuki
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Tehama
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
      • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Huduma za jamii
      • Maadili
      • Fedha, Utawala, na Mipango
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Kujua Sheria
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za Ofisi au Kitaifa
      • YOUTUBE
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

OFISI YA MKUU WA WILAYA YAENDESHA SEMINA KWA WATUMISHI WA UMMA

Posted on: January 30th, 2025

Watumishi wilayani Mafia wametakiwa kuwa na nidhamu wawapo kazini pamoja na kuheshimu mamlaka zilizopo. 

Hayo yamesemwa leo Januari 30, 2025 na Katibu Tawala Msaidizi Mkoa wa Pwani Ndg. Peter Bila wakati wa Semina kwa Watumishi wa Umma wilayani Mafia iliyofanyika katika ukumbi wa Halmashauri uliopo Chicco. 

Ndg. Bila ameeleza kwamba watumishi wana wajibu mkubwa kuzingatia weledi na nidhamu wawapo kazini ili waweze kuwatumikia wananchi ipasavyo pamoja na kutii mamlaka. 

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mafia Ndg. Mussa Kitungi amepongeza na kutambua mchango mkubwa wa kuwa na semina na mafunzo kwa watumishi ili kuwaongezea ujuzi katika masuala ya msingi wawapo kazini. 

Ndg. Kitungi ameeleza kuwa suala la maadili kwa watumishi ni la muhimu kupewa kipaumbele na halina budi kuzingatiwa maana miongoni mwa mambo ya kupambana nayo baada ya ujinga, maradhi na umaskini, suala la maadili ni la msingi. 

" Kwa mazingira tuliyonayo kwa sasa, ukiniuliza mimi nitasema maadui wameongezeka, adui wa nne ni ukosefu wa maadili" ameeleza Ndg. Kitungi. 

Aidha, ameelezea umuhimu wa kuwepo kwa  semina hiyo kila mwaka ili kufundisha suala la maadili na  kuahidi kuwa ofisi yake ipo tayari kutoa ushirikiano  kufanikisha hilo. 

Semina hiyo kwa watumishi wa umma imeandaliwa na taasisi mbalimbali za Serikali na zisizo za kiserikali zikiwemo taasisi za kifedha. 

Katibu Tawala wa Wilaya ya Mafia, Ndg. Shabani Shabani amepongeza hatua hiyo na kutambua mchango wake katika kuongeza uwezo wa watumishi katika utendaji kazi akitambua mchango wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi ( WCF), OSHA, TUGHE, Action Aid, Benki za NMB na CRDB kwa kushirikiana na Sekretarieti ya Maadili pamoja na Halmashauri ya Wilaya ya Mafia.


Matangazo

  • TANGAZO LA KUONGEZWA MUDA WA KULIPIA VIWANJA May 20, 2025
  • Tazama zote

Habari za hivi punde

  • WITO WATOLEWA KWA WATOTO WA KIKE KUPENDA MASOMO YA SAYANSI

    May 17, 2025
  • MAFIA KUUNGANISHWA NA UMEME WA GRIDI YA TAIFA

    May 16, 2025
  • WANANCHI WAASWA KUJITOKEZA KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 16, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI LARIDHIA KUANZISHWA KWA MRADI WA UONGEZAJI THAMANI ZAO LA DAGAA

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

MWENGE WA UHURU WAPONGEZA VIWANGO VYA BARABARA YA MSUFINI
Tazama Video zaidi

Viungo vya haraka

  • Home
  • Photo Gallery
  • FAQ
  • Tourism
  • Investment
  • MATOKEO YA STD VII 2022

Viungo vinavyohusiana

  • OR- TAMISEMI
  • OR- Menejimenti Utumishi wa Umma
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Pwani
  • Sekretarieti ya ajira katika Utumishi wa Umma
  • Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi
  • Wizara ya Fedha na Mipango

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Free Visitor&Stat Counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kilindoni-Bomani Street

    Anuani ya posta: 85

    Simu: 0232010199

    Simu ya mkononi:

    Baruapepe: ded.mafia@pwani.go.tz / ded@mafiadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Katazo
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma namba 1
    • YOUTUBE

Copyright ©2017 Mafia District Council . All rights reserved.