• Wasiliana nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mafia District Council
Mafia District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais , Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mafia

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Ardhi, Mipango miji na Maliasili
      • Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
        • Kitengo cha Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Kilimo na Ushirika
      • Ujenzi na Zima Mmoto
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango na Takwimu
    • Vitengo
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ufugaji Nyuki
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Tehama
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
      • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Huduma za jamii
      • Maadili
      • Fedha, Utawala, na Mipango
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Kujua Sheria
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za Ofisi au Kitaifa
      • YOUTUBE
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

SERIKALI YADHAMIRIA KUIFUNGUA MAFIA ZAIDI KWA KUBORESHA MIUNDOMBINU YA USAFIRI

Posted on: December 7th, 2024

Ikiwa ni siku ya pili ya maonesho ya Tamasha la Utalii ( Mafia Island Festival) viongozi kutoka taasisi mbalimbali za Kiserikali na zisizo za serikali, wafanyabiashara, wadau wa utalii pamoja na wananchi kwa ujumla wamejitokeza kushiriki Tamasha hilo kwa kutembelea mabanda ya maonesho. 

Mkuu wa Wilaya ya Kibiti, Kanali Joseph Kolombo ambaye ni mgeni rasmi kwa siku ya leo Desemba 7, 2024 ameelezea umuhimu wa kuboresha miundombinu wilayani Mafia, hasa usafiri wa anga na maji.

"Mafia sasa inaendelea kufunguka, hivyo watalii wanaoingia ni wengi, jukumu letu la msingi lililopo ni kuhakikisha panafikika kwa urahisi" alisema Kanali Kolombo akielezea hali ya usafiri kisiwani ambapo ametoa wito kwa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege kuboresha kiwanja cha ndege kwakuwa hivi sasa safari za ndege haziwezi kufanyika usiku, kwakuwa hakuna taa zinazowezesha ndege kutua usiku.

Aidha, ameelezea umuhimu wa kuboresha usafiri wa majini ili kupunguza changamoto kwa wananchi.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Maendeleo ya Sanaa kutoka Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Asha Salim ameipongeza Wilaya ya Mafia kwa kuandaa Tamasha huku akielezea mchango wake katika kukuza utalii na utamaduni kisiwani Mafia na Taifa kwa ujumla.

" Matamasha kama haya ni muhimu sana katika kuendeleza, kuibua, kukuza utamaduni wetu wa manzanita ikiwemo sanaa" alisema Dkt. Asha

Viongozi mbalimbali wakiongozwa na Kanali Kolombo walipata fursa ya kushuhudia mashindano ya michezo mbalimbali na  kutembelea mabanda ya maonesho kuona bidhaa na huduma zitolewazo na wadau wa utalii, uhifadhi mazingira na wafanyabiashara kwa ujumla, hasa katika masuala ya uchumi wa buluu.

Tamasha hilo linatarajiwa kumalizika ifikapo kesho Desemba 8, 2024.


Matangazo

  • TANGAZO LA KUONGEZWA MUDA WA KULIPIA VIWANJA May 20, 2025
  • Tazama zote

Habari za hivi punde

  • WITO WATOLEWA KWA WATOTO WA KIKE KUPENDA MASOMO YA SAYANSI

    May 17, 2025
  • MAFIA KUUNGANISHWA NA UMEME WA GRIDI YA TAIFA

    May 16, 2025
  • WANANCHI WAASWA KUJITOKEZA KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 16, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI LARIDHIA KUANZISHWA KWA MRADI WA UONGEZAJI THAMANI ZAO LA DAGAA

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

MWENGE WA UHURU WAPONGEZA VIWANGO VYA BARABARA YA MSUFINI
Tazama Video zaidi

Viungo vya haraka

  • Home
  • Photo Gallery
  • FAQ
  • Tourism
  • Investment
  • MATOKEO YA STD VII 2022

Viungo vinavyohusiana

  • OR- TAMISEMI
  • OR- Menejimenti Utumishi wa Umma
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Pwani
  • Sekretarieti ya ajira katika Utumishi wa Umma
  • Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi
  • Wizara ya Fedha na Mipango

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Free Visitor&Stat Counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kilindoni-Bomani Street

    Anuani ya posta: 85

    Simu: 0232010199

    Simu ya mkononi:

    Baruapepe: ded.mafia@pwani.go.tz / ded@mafiadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Katazo
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma namba 1
    • YOUTUBE

Copyright ©2017 Mafia District Council . All rights reserved.