• Wasiliana nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mafia District Council
Mafia District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais , Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mafia

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Ardhi, Mipango miji na Maliasili
      • Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
        • Kitengo cha Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Kilimo na Ushirika
      • Ujenzi na Zima Mmoto
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango na Takwimu
    • Vitengo
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ufugaji Nyuki
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Tehama
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
      • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Huduma za jamii
      • Maadili
      • Fedha, Utawala, na Mipango
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Kujua Sheria
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za Ofisi au Kitaifa
      • YOUTUBE
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

SERIKALI YAJIZATITI KUTATUA CHANGAMOTO ZA WALIMU

Posted on: August 23rd, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Mafia, Mhe. Aziza Mangosongo ameipongeza Serikali kwa kuendelea kutatua changamoto za walimu zikiwemo madeni ya uhamisho na likizo, pamoja na ukosefu wa nyumba za watumishi.

Mhe. Mangosongo ameyasema hayo katika kongamano la walimu wanawake lililofanyika wilayani Mafia leo Agosti 23, 2024.

" Mlinipa taarifa kuhusu changamoto zenu nyingi ikiwemo madeni ya uhamisho, sasa madeni yenu yatalipwa kwa mkupuo maana Mhe. Rais yupo kazini" alisema Mhe. Mangosongo. Kwa mfano, hapo awali kwa shule za sekondari, madeni ya likizo yalikuwa yakitengewa Milioni 14 kwa mwaka, ila sasa hivi ni Milioni 28 na fedha za uhamisho zilitengwa Milioni 16, ila kwa sasa ni Milioni 40.

Mhe. Mangosongo ametumia fursa hiyo pia kuwasisitiza walimu juu ya weledi katika kazi pamoja na kujituma ili kuleta mabadiliko chanya kwa wanafunzi na sekta ya elimu nchini.

"Niwaombe sana walimu maana tunawajua watoto, hivyo tukashirikiane na wazazi na watoto wenyewe ili kuongeza ufaulu na kupunguza changamoto zinginezo zikiwemo ukatili wa kijinsia, utoro na mengineyo"

Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Bi.Tabu Makanga ameishukuru Serikali chini ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kupigania maslahi ya walimu kama vile kuwapandisha madaraja walimu wa Sekondari na Msingi.

Kwa mwaka 2024, walimu 174 wamepanda madaraja; ambapo walimu 114 ni walimu wa shule za msingi na walimu 60 wa sekondari huku Halmashauri kupitia Idara ya Elimu Msingi na Sekondari ikiendelea kuhakikisha walimu wengine wanapata maslahi yao kama kupunguza madeni ya likizo na posho.

" Kwa mwaka wa fedha 2023/ 2024 tumeweza kupunguza madeni ya Milioni 40 kwa walimu wa Sekondari na Milioni 94.86 kwa ajili ya walimu wa shule za msingi" alieleza Bi. Makanga. Miongoni mwa shughuli zilizofanyika katika kongamano hilo ni pamoja na utoaji wa misaada kwa wafungwa pamoja na wagonjwa katika Hospitali ya Wilaya kwa kuwapatia mahitaji mbalimbali.


Matangazo

  • TANGAZO LA KUONGEZWA MUDA WA KULIPIA VIWANJA May 20, 2025
  • Tazama zote

Habari za hivi punde

  • WITO WATOLEWA KWA WATOTO WA KIKE KUPENDA MASOMO YA SAYANSI

    May 17, 2025
  • MAFIA KUUNGANISHWA NA UMEME WA GRIDI YA TAIFA

    May 16, 2025
  • WANANCHI WAASWA KUJITOKEZA KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 16, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI LARIDHIA KUANZISHWA KWA MRADI WA UONGEZAJI THAMANI ZAO LA DAGAA

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

MWENGE WA UHURU WAPONGEZA VIWANGO VYA BARABARA YA MSUFINI
Tazama Video zaidi

Viungo vya haraka

  • Home
  • Photo Gallery
  • FAQ
  • Tourism
  • Investment
  • MATOKEO YA STD VII 2022

Viungo vinavyohusiana

  • OR- TAMISEMI
  • OR- Menejimenti Utumishi wa Umma
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Pwani
  • Sekretarieti ya ajira katika Utumishi wa Umma
  • Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi
  • Wizara ya Fedha na Mipango

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Free Visitor&Stat Counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kilindoni-Bomani Street

    Anuani ya posta: 85

    Simu: 0232010199

    Simu ya mkononi:

    Baruapepe: ded.mafia@pwani.go.tz / ded@mafiadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Katazo
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma namba 1
    • YOUTUBE

Copyright ©2017 Mafia District Council . All rights reserved.