• Wasiliana nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mafia District Council
Mafia District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais , Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mafia

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Ardhi, Mipango miji na Maliasili
      • Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
        • Kitengo cha Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Kilimo na Ushirika
      • Ujenzi na Zima Mmoto
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango na Takwimu
    • Vitengo
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ufugaji Nyuki
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Tehama
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
      • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Huduma za jamii
      • Maadili
      • Fedha, Utawala, na Mipango
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Kujua Sheria
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za Ofisi au Kitaifa
      • YOUTUBE
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

SERIKALI YASISITIZA USHINDANI SOKO LA MWANI MAFIA

Posted on: October 6th, 2025

Mkuu wa Wilaya ya Mafia ameelekeza kuwa soko la mwani wilayani Mafia ni huru na hivyo Serikali inaruhusu ushindani wa wanunuzi wa zao hilo kwa kuzingatia sheria na miongozo iliyopo katika soko bila vipingamizi vya mtu mmojammoja au kampuni. 

Mhe. Mangosongo ameyasema hayo leo Oktoba 6, 2025 wakati wa kikao chake na wadau wa mwani wilayani Mafia kilicholenga kujadili na kusikiliza kero za wakulima wa zao hili ili kuweka mikakati stahiki ya kutatua changamoto zilizopo, hasa kuwepo kwa mnunuzi mmoja mkubwa wa zao hilo kisiwani Mafia ambaye ni kampuni ya 'Mwani Mariculture'.

" Sisi kama Mafia tunaenda na azimio la kufungua mipaka ya wanunuzi ili waje kununua mwani Mafia, na kingine tunataka taratibu zifuatwe, chochote kitakachokuwa kinapelekwa kwa wakulima, kipite Halmashauri ili Idara ya Kilimo wakione. Lengo letu wakulima wanufaike na bei kupanda kutoka Shilingi 800 kwa Kilo hadi kufikia Shilingi 1000" alieleza Mhe. Mangosongo akisisitiza ushindani kakika soko la mwani.

Awali, akiwasilisha taatifa ya mwenendo wa zao la mwani, Afisa Uvuvi wa Wilaya Ndugu Alfahad Mohamed alieleza kuwa katika mwaka wa fedha 2024/ 2025, mavuno ya mwani yalikuwa ni Tani 600 zenye thamani ya Shilingi Milioni 420 kwa bei ya Shilingi 700 kwa kilo huku asilimia 90 ya wakulima wa zao hilo ikiwa ni wanawake.

Kwa upande wake, Mhifadhi Shirikishi Jamii, Hifadhi ya Bahari Mafia( HIBAMA) Ndugu Albert Makalla, ameeleza jitihada za taasisi hiyo katika kuhakikisha wakulima wa mwani wanaongeza thamani ya zao hilo kwa kutoa mafunzo kupitia wataalam mbalimbali ndani ya Wilaya na nje ya Wilaya na kutoa wito kwa wakulima kuchangamkia fursa za mafunzo pale zinapotokea.

Wakulima wa mwani kutoka maeneo mbalimbali wilayani Mafia wameishukuru Serikali kupitia ofisi ya Mkuu wa Wilaya kwa kuwakutanisha na kuweka mikakati ya kuboresha zao hilo kwa kutatua changamoto wanazokumbana nazo.

" Tunaishukuru Serikali na Ofisi yako kwa jambo hili, ila tunaomba mtusaidie maana tuna changamoto sana ya vitendea kazi pamoja na ujuzi wa kupanda zao hili" alieleza Bi. Rabihu Hemedi, mkulima wa mwani kutoka kijiji cha Banja.

Imebainika kuwa, elimu ni jambo muhimu katika kuhakikisha zao hilo linaboreshwa na kupanda thamani ili kukuza soko lake ambalo halijawa na mwenendo mzuri kama inavyotakiwa pamoja na kuunda ushirika ili kuleta suluhisho. 

" Nashukuru sana kwa kikao hiki adhimu na muhimu pia kuweza kumuomba Mkuu wa Wilaya atusaidie kupitia wataalam ili tupate ujuzi kuhusu upandaji mwani, pia tunaomba mchakato wa uanzishwaji wa ushirika ili tuweze kukwamuka" alieleza Bw. Nasri Basha, mkulima wa mwani kutoka kijiji cha Kiegeani.

Katika hatua nyingine, Mhe. Mangosongo amewataka wataalam kuhakikisha wanapata takwimu sahihi kuhusu wakulima wa mwani waliopo pamoja na hali ya zao hilo kwa ujumla ili kuweka mikakati yenye uhalisia kuboresha zao hilo.


Matangazo

  • MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO; WASIMAMIZI WASAIDIZI NA MAKARANI (UCHAGUZI MKUU, 2025) October 20, 2025
  • Tazama zote

Habari za hivi punde

  • WAVUVI NA WAMILIKI WA VYOMBO WAASWA KUZINGATIA SHERIA KUEPUKA MIGOGORO NA SERIKALI

    October 17, 2025
  • MAFIA YAADHIMISHA JUMA LA ELIMU YA WATU WAZIMA

    October 09, 2025
  • UGAWAJI WA VYANDARUA WAZINDULIWA WILAYANI MAFIA

    October 08, 2025
  • SERIKALI YASISITIZA USHINDANI SOKO LA MWANI MAFIA

    October 06, 2025
  • Tazama zote

Video

USIKOSE KUWA SEHEMU YA TUKIO HILI MUHIMU KIHISTORIA
Tazama Video zaidi

Viungo vya haraka

  • Home
  • Photo Gallery
  • FAQ
  • Tourism
  • Investment
  • MATOKEO YA STD VII 2022

Viungo vinavyohusiana

  • OR- TAMISEMI
  • OR- Menejimenti Utumishi wa Umma
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Pwani
  • Sekretarieti ya ajira katika Utumishi wa Umma
  • Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi
  • Wizara ya Fedha na Mipango

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Free Visitor&Stat Counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kilindoni-Bomani Street

    Anuani ya posta: 85

    Simu: 0232010199

    Simu ya mkononi:

    Baruapepe: ded.mafia@pwani.go.tz / ded@mafiadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Katazo
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma namba 1
    • YOUTUBE

Copyright ©2017 Mafia District Council . All rights reserved.