• Wasiliana nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mafia District Council
Mafia District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais , Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mafia

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Ardhi, Mipango miji na Maliasili
      • Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
        • Kitengo cha Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Kilimo na Ushirika
      • Ujenzi na Zima Mmoto
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango na Takwimu
    • Vitengo
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ufugaji Nyuki
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Tehama
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
      • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Huduma za jamii
      • Maadili
      • Fedha, Utawala, na Mipango
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Kujua Sheria
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za Ofisi au Kitaifa
      • YOUTUBE
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

TANROADS MAFIA YATAKIWA KUTENGENEZA MITARO KUKABILIANA NA KUTUAMA KWA MAJI YANAYOZALISHA MBU

Posted on: September 1st, 2025

Mkuu wa Wilaya ya Mafia Mhe. Aziza Mangosongo ameielekeza Wakala ya Barabara Tanzania ( TANROADS) wilayani Mafia kutengeneza mitaro itakayosaidia kuondosha maji ambayo yamekuwa yakituama katika maeneo mbalimbali  kwa muda mrefu na kuleta kero kwa wakazi pamoja na kupelekea kuongezeka kwa mazalia ya mbu. 

Akitoa maelekezo hayo leo Septemba Mosi, 2025 wakati wa kikao cha kutambulisha msambazaji wa vyandarua ambaye ni Bohari ya Dawa ( MSD), Mhe. Mangosongo ameitaka TANROADS kuhakikisha kuwa inaweka miundombinu mizuri itakayosaidia kumalizika kwa tatizo la maji kutuama hasa katika maeneo ya pembezoni mwa barabara, maeneo ya Hospitali na makazi ya watu.

" Barabara nyingi au sehemu nyingi zina madimbwi ila hatuna mifereji, hivyo madimbwi haya yatengenezewe mifereji ili maji yasituame na kuweza kutengeneza vimelea vya mbu" alisisitiza.

Kwa upande wake, Mratibu wa Malaria wa Mkoa wa Pwani Dkt. Themistocles Nyeme ameeleza kuwa zaidi ya vyandarua 1,200,000 vinatarajiwa kusambazwa mkoani Pwani ikijumuisha halmashauri saba ambazo zina maambukizi makubwa ya malaria ikiwemo wilaya ya Mafia.

Hatua hiyo inatarajiwa kupunguza kwa kiasi kikubwa maambukizi ya malaria wilayani Mafia na mkoa wa Pwani kwa ujumla.

Kiwango cha maambukizi ya malaria mkoani pwani kwa hivi sasa ni asilimia 6.7 ikilinganishwa na asilimia 14 kwa mwaka 2022.

" Kwa Halmashauri yetu pia, kiwango cha maambukizi ya malaria ni asilimia 6.7, hivyo tunatoa wito kwa wananchi kujikita katika njia mbalimbali za kujikinga na malaria ikiwemo kutumia vyandarua, kuwahi kufika katika vituo vya kutolea huduma ya afya mara tu wapatapo dalili za malaria pamoja na kuzingatia usafi wa mazingira " alieleza Bi. Rukia Maumba, Mratibu wa Malaria wilaya ya Mafia.

Katika hatua nyingine, wahudumu wa afya wamesisitizwa kuwa zoezi la ugawaji wa vyandarua liende sambamba na utoaji wa elimu kwa jamii juu ya namna bora ya kuzuia maambukizi ya malaria pamoja na kutumia vyandarua hivyo kwa lengo lililokusudiwa. Zaidi ya vyandarua 48,000 vinatarajiwa kusambazwa katika kaya 21,100 zilizosajiliwa wilayani Mafia.


Matangazo

  • MWALIKO WA KUHUDHURIA BARAZA LA KWANZA LA MADIWANI November 29, 2025
  • Tazama zote

Habari za hivi punde

  • CHUO CHA VETA MAFIA CHATOA WAHITIMU KWA MARA YA KWANZA TANGU KUANZISHWA

    November 23, 2025
  • WITO WATOLEWA KWA WADAU KUSHIRIKIANA NA SERIKALI KUBORESHA ELIMU

    November 21, 2025
  • JITIHADA ZAIDI ZAHITAJIKA KUBORESHA MASUALA YA LISHE WILAYANI MAFIA

    November 14, 2025
  • WANUFAIKA WAASWA KUTUMIA MIKOPO YA ASILIMIA 10 KWA MALENGO YALIYOKUSUDIWA

    November 13, 2025
  • Tazama zote

Video

USIKOSE KUWA SEHEMU YA TUKIO HILI MUHIMU KIHISTORIA
Tazama Video zaidi

Viungo vya haraka

  • Home
  • Photo Gallery
  • FAQ
  • Tourism
  • Investment
  • MATOKEO YA STD VII 2022

Viungo vinavyohusiana

  • OR- TAMISEMI
  • OR- Menejimenti Utumishi wa Umma
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Pwani
  • Sekretarieti ya ajira katika Utumishi wa Umma
  • Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi
  • Wizara ya Fedha na Mipango

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Free Visitor&Stat Counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kilindoni-Bomani Street

    Anuani ya posta: 85

    Simu: 0232010199

    Simu ya mkononi:

    Baruapepe: ded.mafia@pwani.go.tz / ded@mafiadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Katazo
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma namba 1
    • YOUTUBE

Copyright ©2017 Mafia District Council . All rights reserved.