• Wasiliana nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mafia District Council
Mafia District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais , Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mafia

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Ardhi, Mipango miji na Maliasili
      • Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
        • Kitengo cha Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Kilimo na Ushirika
      • Ujenzi na Zima Mmoto
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango na Takwimu
    • Vitengo
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ufugaji Nyuki
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Tehama
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
      • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Huduma za jamii
      • Maadili
      • Fedha, Utawala, na Mipango
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Kujua Sheria
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za Ofisi au Kitaifa
      • YOUTUBE
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

TEKNOLOJIA MPYA KUONGEZA THAMANI ZAO LA DAGAA WILAYANI MAFIA

Posted on: April 16th, 2025

Wafanyabiashara wa dagaa wilayani Mafia wanatarajia kunufaika na mradi wa uongezaji wa thamani wa bidhaa hiyo utakaosaidia kukuza soko pamoja na kukuza kipato Chao. 

Lengo la mradi huo ni kuongeza uelewa na matumizi ya uzalishaji kwa mfumo gatuliwa wa nishati jadidifu ( Jua) ili kuongeza ufanisi katika uzalishaji, uchakataji, uongeza thamani na kupunguza upotevu wa zao la dagaa na mnyororo wa thamani wilayani Mafia. 

" Tulihamasika na kuungana na wadau wengine ili kuja na mradi utakaobadilisha maisha ya wananchi. Hii ni kutokana na kuwepo kwa changamoto kadhaa katika soko la dagaa" alieleza Mkurugenzi Mkazi wa WWF Tanzania,  Dr. Amani Ngusaru. Tuna matumaini kuwa mradi huu utafanya Mafia kuwa sehemu inayoongoza nchini kwa uzalishaji wa dagaa" aliongeza. 

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Mafia Mhe. Aziza Mangosongo amewashukuru wananchi wakiongozwa na Serikali ya  kijiji cha Chunguruma ambapo mradi utatekelezwa, kwa kutoa eneo la mradi ili kuhakikisha wafanyabiashara wanaondokana na changamoto ambazo zimekuwa zikiwakabili. 

Utekelezaji wa mradi huo utaokoa asilimia 35 ya thamani ya dagaa inayopotea wakati wa uchakataji. 

"Mradi huu utatunufaisha na utatufanya tuingie kwenye ushindani mkubwa katika soko kutokana na ubora wa bidhaa zetu. Tumekuwa tukitumia chanja kuanika dagaa, ambapo kipindi cha mvua, tunapata hasara kulinganisha na kipindi cha jua wakati ambao ndoo ndogo ya dagaa inauzwa kwa Shilingi elfu 50 ila kipindi cha mvua, uanikaji wa dagaa unakuwa mgumu kupelekea dagaa kuharibika, hata bei ya ndoo ndogo hupungua na kufika hadi elfu 15" alieleza Hashim Kirama, Mwenyekiti wa  CHAWASA, Mafia. 

Kisiwa cha Mafia kinazalisha asilimia 40 ya dagaa wote wanaovuliwa katika ukanda wa bahari ya Hindi, hivyo uwepo wa mradi huu utafanya Mafia iendelee kuzalisha dagaa wengi zaidi kutokana na ubora wa uchakataji pamoja na utunzaji wa mazingira. 

Mradi huu unatekelezwa na Shirika la Uhifadhi wa Mazingira Duniani ( WWF) kwa kushirikiana na wadau mbalimbali kama mashirika na taasisi za Kiserikali na zisizo za kiserikali ikiwemo WorldFish, TAFIRI Halmashauri ya Wilaya ya Mafia, FETA), CHAWASA, na wananchi ambao wote kwa pamoja wana mchango mkubwa kuleta maendeleo.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUFUNGULIWA KWA DIRISHA LA UTOAJI WA MIKOPO May 02, 2025
  • Tazama zote

Habari za hivi punde

  • MENEJIMENTI YA HALMASHAURI YASISITIZA USIMAMIZI MZURI WA MIRADI YA MAENDELEO

    April 23, 2025
  • TEKNOLOJIA MPYA KUONGEZA THAMANI ZAO LA DAGAA WILAYANI MAFIA

    April 16, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPONGEZA UBORA WA BARABARA KITONGOJI CHA MSUFINI

    April 08, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAWASILI WILAYANI MAFIA

    April 07, 2025
  • Tazama zote

Video

MWENGE WA UHURU WAPONGEZA VIWANGO VYA BARABARA YA MSUFINI
Tazama Video zaidi

Viungo vya haraka

  • Home
  • Photo Gallery
  • FAQ
  • Tourism
  • Investment
  • MATOKEO YA STD VII 2022

Viungo vinavyohusiana

  • OR- TAMISEMI
  • OR- Menejimenti Utumishi wa Umma
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Pwani
  • Sekretarieti ya ajira katika Utumishi wa Umma
  • Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi
  • Wizara ya Fedha na Mipango

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Free Visitor&Stat Counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kilindoni-Bomani Street

    Anuani ya posta: 85

    Simu: 0232010199

    Simu ya mkononi:

    Baruapepe: ded.mafia@pwani.go.tz / ded@mafiadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Katazo
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma namba 1
    • YOUTUBE

Copyright ©2017 Mafia District Council . All rights reserved.