• Wasiliana nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mafia District Council
Mafia District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais , Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mafia

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Ardhi, Mipango miji na Maliasili
      • Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
        • Kitengo cha Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Kilimo na Ushirika
      • Ujenzi na Zima Mmoto
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango na Takwimu
    • Vitengo
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ufugaji Nyuki
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Tehama
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
      • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Huduma za jamii
      • Maadili
      • Fedha, Utawala, na Mipango
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Kujua Sheria
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za Ofisi au Kitaifa
      • YOUTUBE
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

UKOSEFU WA ELIMU MIONGONI MWA VYANZO ZINAVYOSABABISHA VIFO VYA WAZAZI NA WATOTO

Posted on: May 29th, 2025

Wito umetolewa kwa wahudumu wa afya kuweka mkazo katika utoaji wa elimu kwenye jamii kuhusu umuhimu wa mama wajawazito kuhudhuria kliniki kwa wakati pamoja na kujifungulia katika vituo vya kutolea huduma za afya ili kuepuka vifo vitokanavyo na uzazi na watoto wachanga.

Wito huo umetolewa leo Mei 29, 2025 wakati wa kikao cha kujadili viashiria vinavyosababisha vifo vitokanavyo na uzazi na watoto wachanga kwa lengo la kuweka mikakati ya kuondokana na tatizo hilo.

Akizungumza katika kikao hicho, Mwenyekiti wa Kamati ya Huduma za Jamii ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Ndagoni Mhe. Mohammed Rashid amewataka wataalam wa afya kuongeza nguvu katika kutembelea jamii ili waweze kutoa elimu kuhusu afya ya uzazi.

" Tumeona tatizo jubwa zaidi ni elimu, elimu ya kutosha haijaifikia jamii hasa kina mama ili kujua umuhimu wa kuhudhuria kliniki mapema na kwenda na mwenza" ameeleza Mhe. Rashid. " Hivyo kwa pamoja tumekubaliana kuwa wataalam washuke kwenda kuwapa elimu ya kutosha kuhusu elimu hii pamoja na kuweka wazi Sera ya afya kuhusu utoaji wa huduma za afya kwa mama wajawazito na watoto wachanga" aliongeza.Akieleza hali ya afya ya uzazi wilayani, Mratibu wa Afya ya Uzazi na Mtoto wilaya ya Mafia Bi. Mwanahawa Kassim amesema kwamba changamoto kubwa inayopelekea vifo vya wazazi na watoto wachanga ni kuchelewa kuanza kliniki kwa wajawazito pamoja na wajawazito kutojifungulia vituoni.


"Kwa kipindi cha kipindi cha Januari hadi Aprili mwaka huu, tumepata wajawazito wapya 686, lakini waliowahi kliniki ni 86 tu ambao ni asilimia 12.5 ambayo ni mbaya sana na lengo la Taifa ambalo linataka asilimia 95 ya wajawazito kuwahi kliniki" alieleza Bi. Kassim

Aidha, amesisitiza umuhimu wa wanaume kuwajibika kwa kuhakikisha wanawapeleka wenza wao kliniki pindi wanapopata ujauzito ili elimu italowayo vituoni iwafikie wote na kusaidia kupunguza changamoto zinazoweza kujitokeza.

Kati ya wajawazito waliofika kituoni kwa kipindi hicho ( Januari - Aprili), wajawazito waliosindikizwa na wenza wao ni 445 ambao ni sawa na asilimia 64.8 ambayo ni chini ya lengo lililokisudiwa la kufika asilimia 95.

" Kwa upande wa jamii, naomba nitoe rai kwa kina mama wajawazito kujitahidi kufika kliniki mapema wakiwa na wenza wao ili kupata elimu kuhusu hali za hatari na namna ya kukabiliana nazo, pia kwa Serikali nawaomba watutengenezee miundombinu maana barabarq zikipitika vizuri, mama wajawazito watafika hospitali kwa wakati" alisema Bi. Neema Boaz, Afisa Mtendaji wa kijiji cha Banja.

Katika kipindi cha miezi minne, Januari hadi Aprili 2025, kati ya wazazi 487 waliojifungua, 10 wamejifungulia njiani ambao ni sawa na asilimia mbili (2), huku changamoto nyingine ikiwa ni saratani ya mlango wa kizazi kwa wanawake inayopelekea vifo kwao.

Kwa kipindi cha miezi minne, wanawake 65 tu walijitokeza kupima saratani ya mlango wa kizazi ambayo ni asilimia 29 ya wazazi, tatizo ambalo wataalam wa afya wameendelea kutoa wito kwa kina mama kufanya vipimo mapema ili kuzuia hatari zinazoweza jitokeza pindi wanapokutwa na matatizo ya saratani pamoja na maambukizi mengine kama Virusi Vya UKIMWI.


Matangazo

  • TANGAZO LA KUONGEZWA MUDA WA KULIPIA VIWANJA May 20, 2025
  • Tazama zote

Habari za hivi punde

  • UKOSEFU WA ELIMU MIONGONI MWA VYANZO ZINAVYOSABABISHA VIFO VYA WAZAZI NA WATOTO

    May 29, 2025
  • MRADI WA KUTUNZA MSITU WA MLOLA WAWAZINDULIWA RASMI WILAYANI MAFIA

    May 26, 2025
  • WATUMISHI WAASWA KUZINGATIA MAADILI WAWAPO KAZINI

    May 24, 2025
  • KIJIJI CHA DONGO KUPATA KITUO CHA AFYA

    May 23, 2025
  • Tazama zote

Video

MWENGE WA UHURU WAPONGEZA VIWANGO VYA BARABARA YA MSUFINI
Tazama Video zaidi

Viungo vya haraka

  • Home
  • Photo Gallery
  • FAQ
  • Tourism
  • Investment
  • MATOKEO YA STD VII 2022

Viungo vinavyohusiana

  • OR- TAMISEMI
  • OR- Menejimenti Utumishi wa Umma
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Pwani
  • Sekretarieti ya ajira katika Utumishi wa Umma
  • Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi
  • Wizara ya Fedha na Mipango

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Free Visitor&Stat Counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kilindoni-Bomani Street

    Anuani ya posta: 85

    Simu: 0232010199

    Simu ya mkononi:

    Baruapepe: ded.mafia@pwani.go.tz / ded@mafiadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Katazo
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma namba 1
    • YOUTUBE

Copyright ©2017 Mafia District Council . All rights reserved.