• Wasiliana nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mafia District Council
Mafia District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais , Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mafia

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Ardhi, Mipango miji na Maliasili
      • Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
        • Kitengo cha Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Kilimo na Ushirika
      • Ujenzi na Zima Mmoto
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango na Takwimu
    • Vitengo
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ufugaji Nyuki
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Tehama
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
      • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Huduma za jamii
      • Maadili
      • Fedha, Utawala, na Mipango
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Kujua Sheria
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za Ofisi au Kitaifa
      • YOUTUBE
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

UTENGAJI WA MAENEO YA MALISHO SULUHISHO LA MIGOGORO KATI YA WAKULIMA NA WAFUGAJI

Posted on: September 24th, 2025

Mkuu wa Wilaya ya Mafia Mhe. Aziza Mangosongo ameitaka Halmashauri kutenga maeneo maalum kwa ajili ya malisho ya mifugo ili kuepusha migogoro inayoweza kujitokeza kati ya wafugaji na wakulima.

Mhe. Mangosongo ametoa agizo hile leo Septemba 24, 2025 akiwa eneo la Kibaoni kata ya Kiegeani wakati wa hafla ya uhamasishaji wa utoaji wa chanjo kwa mafugo ambapo chanjo zilizotolewa ni pamoja na chanjo ya homa ya mapafu kwa ng'ombe, sotoka kwa mbuzi na kondoo pamoja na chanjo ya kideri au mdondo, ndui na mafua ya kuku kwa kuku wa kienyeji.

Mhe. Mangosongo ameeleza kuwa ni muhimu kwa wafugaji na wakulima kuishi kwa amani na upendo na njia mojawapo ya kuhakikisha migogoro inatoweka ni kwa wafugaji kuwa na maeneo maalum kwa ajili ya malisho ya mifugo yao.

" Ni vyema zaidi wafugaji waandaliwe maeneo maalum kwa ajili ya maeneo ya malisho wasiwe kama wametelekezwa na kupelekea mifugo yao kuzagaa maeneo ya mjini na katika mashamba ya watu" alieleza.

Aidha, amewataka wafugaji pamoja na jamii kwa ujumla kuwa makini kwa kutoshiriki katika tabia ya wizi wa mifugo ambayo ni kinyume na sheria ambapo ameeleza kuwa hatua kali za kisheria zitachukuliwa kwa yeyote atakayejihusisha na wizi wa mifugo.

Amesisitiza kuwa ni muhimu kwa wafugaji kuwa na zizi la mifugo katika maeneo yao ili kuepusha wizi, mifugo kuingia katika mashamba ya wakulima pamoja na kusambaa kwa mifugo , huku akiwataka maafisa ugani kufanya ukaguzi kuhakikisha agizo linatekelezwa.

Kwa upande wake, Mkuu wa Idara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi Dkt. Seleman Kataga ametoa wito kwa wafugaji kujitokeza katika zoezi hilo la chanjo ili kudhibiti milipuko ya magonjwa na kuongeza uzalishaji wa mifugo na mazao ya mifugo yenye ubora.

Zoezi la chanjo kitaifa linakwenda sambamba na zoezi la utambuzi wa mifugo kielektroniki ambapo Serikali imetenga jumla ya Shilingi Bilioni 216 kipindi cha 2025/2026 zinazofanikisha Serikali kuchangia nusu ya gharama ya chanjo hizo.

Halmashauri ya Wilaya ya Mafia imepokea kiasi cha dozi 49,600 za chanjo zote ikiwa dozi 40,000 ni chanjo za kuku, dozi 8,000 za ng'ombe na dozi 1,600 za mbuzi na kondoo ambapo hadi kufikia sasa kuku 36, 137 wamechanjwa ikifikisha asilimia 90 ya uchanjaji wa kuku, huku zoezi la uchanjaji wa ng'ombe linaendelea ambapo ng'ombe 117 wamechanjwa.


 







Matangazo

  • MWALIKO WA KUHUDHURIA BARAZA LA KWANZA LA MADIWANI November 29, 2025
  • Tazama zote

Habari za hivi punde

  • CHUO CHA VETA MAFIA CHATOA WAHITIMU KWA MARA YA KWANZA TANGU KUANZISHWA

    November 23, 2025
  • WITO WATOLEWA KWA WADAU KUSHIRIKIANA NA SERIKALI KUBORESHA ELIMU

    November 21, 2025
  • JITIHADA ZAIDI ZAHITAJIKA KUBORESHA MASUALA YA LISHE WILAYANI MAFIA

    November 14, 2025
  • WANUFAIKA WAASWA KUTUMIA MIKOPO YA ASILIMIA 10 KWA MALENGO YALIYOKUSUDIWA

    November 13, 2025
  • Tazama zote

Video

USIKOSE KUWA SEHEMU YA TUKIO HILI MUHIMU KIHISTORIA
Tazama Video zaidi

Viungo vya haraka

  • Home
  • Photo Gallery
  • FAQ
  • Tourism
  • Investment
  • MATOKEO YA STD VII 2022

Viungo vinavyohusiana

  • OR- TAMISEMI
  • OR- Menejimenti Utumishi wa Umma
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Pwani
  • Sekretarieti ya ajira katika Utumishi wa Umma
  • Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi
  • Wizara ya Fedha na Mipango

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Free Visitor&Stat Counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kilindoni-Bomani Street

    Anuani ya posta: 85

    Simu: 0232010199

    Simu ya mkononi:

    Baruapepe: ded.mafia@pwani.go.tz / ded@mafiadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Katazo
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma namba 1
    • YOUTUBE

Copyright ©2017 Mafia District Council . All rights reserved.