• Wasiliana nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mafia District Council
Mafia District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais , Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mafia

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Ardhi, Mipango miji na Maliasili
      • Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
        • Kitengo cha Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Kilimo na Ushirika
      • Ujenzi na Zima Mmoto
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango na Takwimu
    • Vitengo
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ufugaji Nyuki
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Tehama
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
      • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Huduma za jamii
      • Maadili
      • Fedha, Utawala, na Mipango
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Kujua Sheria
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za Ofisi au Kitaifa
      • YOUTUBE
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

VETA YATOA MAFUNZO KWA MAMA LISHE ZAIDI YA 200 WA KATA YA KILINDONI

Posted on: June 17th, 2025

Chuo cha Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi wilayani Mafia ( VETA) kimeandaa mafunzo ya ujasiriamali kwa mama lishe na baba lishe wa kata ya Kilindoni yenye lengo la kuwaongezea ujuzi katika masuala mbalimbali yatakayowasaidia kuboresha  biashara zao. 

Akifungua mafunzo hayo Juni 17, 2025, Mkuu wa Wilaya ya Mafia Mhe. Aziza Mangosongo ametoa pongezi kwa chuo cha VETA kwa kuandaa mafunzo hayo na kueleza kuwa Serikali itaendelea kushirikiana na wajasiriamali ili kuwawezesha katika masuala ya kiuchumi. 

Kwa upande wake, Mkuu wa Chuo cha VETA wilaya ya Mafia Ndugu Salim Jumbe ametoa wito kwa wananchi kujitokeza pindi mafunzo mbalimbali yanapoendeshwa ili waweze kupata mbinu mpya na sahihi ambazo zitawasaidia kukuza biashara zao. 

" Tumekuwa tukiendesha mafunzo mbalimbali kwa makundi tofauti kama vile waendesha bodaboda, mafundi ujenzi na waongoza utalii katika chuo chetu, natoa wito kwa wananchi hasa vijana kuchangamkia fursa za mafunzo yanayotolewa na VETA kwa kushiriki kozi za muda mrefu au muda mfupi" alieleza Ndugu Jumbe. 

Washiriki wa mafunzo hayo wamekishukuru chuo cha VETA kwa kushirikiana na Halmashauri ya Wilaya ya Mafia kwa kuandaa mafunzo hayo ambayo wanaimani yataleta mabadiliko katika shughuli zao za kutafuta kipato. 

" Naishukuru sana Serikali kwa kutuandalia mafunzo, tumekuwa tukiona wenzetu wa bodaboda wakipewa mafunzo ila sasa hivi na sisi tumefikiwa, natoa wito kwa kina mama wenzangu kujitokeza ili tushiriki wote" alisema Moza Kazumari, mama lishe kutoka Kilindoni. 

Mada mbalimbali zinatolewa ikiwemo masuala ya afya kwa kuzingatia usafi kwenye biashara, mada kuhusu utunzaji wa mazingira, ujasiriamali pamoja na umuhimu wa kuzingatia lishe bora. 

Washiriki zaidi ya 200 wanatarajia kunufaika na mafunzo hayo yanayoendeshwa kwa siku tano kuanzia Juni 17 hadi 21, 2025.


Matangazo

  • TANGAZO: NAFASI ZA KAZI ZA MUDA; UCHAGUZI MKUU July 02, 2025
  • Tazama zote

Habari za hivi punde

  • VETA YATOA MAFUNZO KWA MAMA LISHE ZAIDI YA 200 WA KATA YA KILINDONI

    June 17, 2025
  • JITIHADA ZIONGEZWE KUTOKOMEZA MALARIA

    June 17, 2025
  • MARUFUKU UTOAJI WA AJIRA KWA WATOTO; AONYA DC MANGOSONGO

    June 16, 2025
  • WANANCHI WAASWA KUJALI AFYA ZAO KUEPUKA MADHARA MAKUBWA YANAYOWEZA KUTOKEA

    June 14, 2025
  • Tazama zote

Video

MWENGE WA UHURU WAPONGEZA VIWANGO VYA BARABARA YA MSUFINI
Tazama Video zaidi

Viungo vya haraka

  • Home
  • Photo Gallery
  • FAQ
  • Tourism
  • Investment
  • MATOKEO YA STD VII 2022

Viungo vinavyohusiana

  • OR- TAMISEMI
  • OR- Menejimenti Utumishi wa Umma
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Pwani
  • Sekretarieti ya ajira katika Utumishi wa Umma
  • Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi
  • Wizara ya Fedha na Mipango

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Free Visitor&Stat Counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kilindoni-Bomani Street

    Anuani ya posta: 85

    Simu: 0232010199

    Simu ya mkononi:

    Baruapepe: ded.mafia@pwani.go.tz / ded@mafiadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Katazo
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma namba 1
    • YOUTUBE

Copyright ©2017 Mafia District Council . All rights reserved.