• Wasiliana nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mafia District Council
Mafia District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais , Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mafia

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Ardhi, Mipango miji na Maliasili
      • Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
        • Kitengo cha Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Kilimo na Ushirika
      • Ujenzi na Zima Mmoto
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango na Takwimu
    • Vitengo
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ufugaji Nyuki
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Tehama
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
      • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Huduma za jamii
      • Maadili
      • Fedha, Utawala, na Mipango
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Kujua Sheria
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za Ofisi au Kitaifa
      • YOUTUBE
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

VIJANA WAASWA KUDUMISHA MUUNGANO

Posted on: April 26th, 2025

" Mnalo jukumu kubwa la kudumisha muungano wetu" asema Mhe. Aziza Mangosongo, Mkuu wa Wilaya ya Mafia wakati wa Kongamano la Vijana la Miaka 61 ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lililofanyika leo Aprili 26, 2025 katika ukumbi wa Halmashauri.


Kongamano hilo lililoratibiwa na Idara ya Maendeleo ya Jamii kwa kushirikiana na Idara ya Elimu Sekondari, limehusisha vijana kutoka shule ya Sekondari ya Kilindoni pamoja na chuo cha ufundi VETA.

Mhe. Mangosongo ameeleza kuwa miongoni mwa mambo yanayotuunganisha ni pamoja na ulinzi na usalama, hivyo hatuna budi kuhakikisha tunawajibika kutunza amani iliyopo.


Kwa upande wake, Katibu Tawala wa Wilaya ya Mafia Ndugu Shabani Shabani amewaasa vijana kujitoa kizalendo ili kuleta maendeleo katika Taifa.


"Ili nchi yetu iende vizuri, inabidi software (akili) ifanye kazi vizuri kwa manufaa ya nchi" alisema Ndugu Shabani akisisitiza kwamba kwa kufanya hivyo watakuwa wanaenzi mazuri yote ya waasisi wa nchi.


Aidha, amewaasa vijana kutorubunika na kuhakikisha wale wote ambao hawakujiandikisha, wanatumia haki yao ya msingi kujiandikisha katika daftari la kudumu mara zoezi hilo litakapoanza kwa mara ya pili ili waweze kupiga kura katika uchaguzi mkuu 2025.


Mada mbalimbali zilitolewa ikiwemo uzalendo, mapambano dhidi ya UKIMWI na Ukatili wa kijinsia, matumizi mazuri ya mitandao ya kijamii, kuepuka vitendo vya utovu wa nidhamu, kama matumizi ya dawa za kulevya, na vitendo vingine vya kuvunja sheria.
Kauli mbiu ya Maadhimisho ya Miaka 61 ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa mwaka huu ni " Muungano Wetu ni Fhamana, Heshima na Tunu ya Taifa, Shiriki Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025.

" Hapo mwanzo nilikuwa nikitumia sana kuni na mkaa, ila baada ya kushiriki mafunzo kuhusu matumizi ya jiko la nishati safi, nitakuwa wa kwanza kuhamasisha wenzangu kutumia nishati safi hasa kwa wachakataji wa samaki, mama lishe wenzangu na wengine" alisema Bi. Aisha Salum, mjasiriamali kutoka kata ya Kilindoni.

Hapo awali, Mwenyekiti wa Halmashauri Mhe. Juma Salum alitoa wito kwa wafanyabiashara kutumia fursa hiyo ili kutumia teknolojia mpya ya nishati ya kupikia na kuachana na matumizi ya kuni ambayo yamekuwa si rafiki kwa mazingira.

Majiko hayo yanayotumia mkaa utokanao na mabaki ya vifuu vya nazi, machicha na makumbi ya nazi na mabaki mbalimbali ya mazao ya shambani, yanatarajiwa kuuzwa  kwa bei ya punguzo kutoka Shilingi 125,000 hadi kufikia Shilingi 35,000 kwa wakazi wa Mafia, na baadhi ya majiko yatatolewa bure kama mfano.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUFUNGULIWA KWA DIRISHA LA UTOAJI WA MIKOPO May 02, 2025
  • Tazama zote

Habari za hivi punde

  • WADAU WADHAMIRIA KUONGEZA THAMANI ZAO LA MWANI

    April 30, 2025
  • MAFIA YAADHIMISHA KILELE CHA WIKI YA CHANJO

    April 30, 2025
  • MAFUNZO YA MFUMO WA UKAGUZI YATOLEWA KWA WAKUU WA DIVISHENI NA VITENGO

    April 29, 2025
  • MRADI WA MAJIKO BANIFU WATAMBULISHWA MAFIA

    April 28, 2025
  • Tazama zote

Video

MWENGE WA UHURU WAPONGEZA VIWANGO VYA BARABARA YA MSUFINI
Tazama Video zaidi

Viungo vya haraka

  • Home
  • Photo Gallery
  • FAQ
  • Tourism
  • Investment
  • MATOKEO YA STD VII 2022

Viungo vinavyohusiana

  • OR- TAMISEMI
  • OR- Menejimenti Utumishi wa Umma
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Pwani
  • Sekretarieti ya ajira katika Utumishi wa Umma
  • Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi
  • Wizara ya Fedha na Mipango

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Free Visitor&Stat Counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kilindoni-Bomani Street

    Anuani ya posta: 85

    Simu: 0232010199

    Simu ya mkononi:

    Baruapepe: ded.mafia@pwani.go.tz / ded@mafiadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Katazo
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma namba 1
    • YOUTUBE

Copyright ©2017 Mafia District Council . All rights reserved.