• Wasiliana nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mafia District Council
Mafia District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais , Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mafia

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Ardhi, Mipango miji na Maliasili
      • Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
        • Kitengo cha Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Kilimo na Ushirika
      • Ujenzi na Zima Mmoto
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango na Takwimu
    • Vitengo
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ufugaji Nyuki
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Tehama
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
      • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Huduma za jamii
      • Maadili
      • Fedha, Utawala, na Mipango
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Kujua Sheria
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za Ofisi au Kitaifa
      • YOUTUBE
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

WADAU WA ELIMU WAKUTANA MAFIA

Posted on: February 12th, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Mafia Mhe. Zephania Sumaye ameongoza kikao cha Wadau wa Elimu wilayani Mafia chenye lengo la kujadili kwa pamoja mafanikio yaliyofikiwa katika sekta ya Elimu, changamoto zinazoikabili sekta hiyo pamoja na kutafuta ufumbuzi wa kudumu juu ya changamoto hizo.  

Akifungua kikao hicho leo Februari 12, Mhe.Sumaye amewaambia wajumbe na wadau wa kikao hicho kuwa suala la elimu ni miongoni mwa haki za msingi za binadamu na hivyo wanapokaa na kujadili maendeleo ya elimu, wanaimarisha misingi ya haki za binadamu.  


Mhe. Sumaye ameongeza kuwa wakati suala la elimu likijadiliwa wilayani Mafia, lionekane kuwa ni jambo litakaloleta mabadiliko si tu kwa Tanzania bali bara zima la Afrika na kusisitiza kuwa  misaada yenye kudhalilisha utu wa Watanzania haina nafasi.


Akisoma Taarifa ya Elimu Wilayani Mafia, Afisa Taaluma Elimu Msingi na Awali ndugu Ephata Kaale ameeleza  kuwa ufaulu kwa shule za Sekondari kidato cha nne umepanda kutoka asilimia 89.1 mwaka 2022 mpaka asilimia 96.1% wakati kwa upande wa elimu msingi ufaulu kwa darasa la saba kwa mwaka 2023 umeshuka kwa asilimia 8 ikilinganishwa na mwaka 2022.


Pamoja na kujadili suala la ufaulu, wadau wa elimu kwa pamoja walipata nafasi ya kujadili changamoto ya upungufu wa madawati, viti na meza  na kuazimia kuchanga kwa hali na mali kuhakikisha changamoto hiyo inakuwa historia.  

Aidha wadau wameazimia kuwekwa kwa sheria ndogo juu ya suala la kuchangia chakula shuleni pamoja na Kushauri kuwa jamii ihamasishwe  kuchanga fedha kwa ajili ya kugharamikia posho ya walimu wa kujitolea ikiwa ni hatua ya kukabiliana na changamoto ya uhaba wa walimu wakati Serikali ikiendelea na juhudi za kuajiri walimu wapya.


Katika hatua nyingine, Mkuu wa Wilaya ya Mafia amepiga marufuku ufanyikaji wa biashara ya vyakula katika maeneo yote ya shule za msingi na sekondari wilayani Mafia na kuwataka wazazi kuweka jitihada katika kuwapatia watoto wao chakula cha mchana.


Zawadi mbalimbali zimetolewa kwa wadau waliotoa michango yao katika mafanikio ya kitaaluma kwa mwaka 2023 huku shule zilizofanya vizuri kitaaluma nazo zikipatiwa tuzo za vyeti na ngao.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUONGEZWA MUDA WA KULIPIA VIWANJA May 20, 2025
  • Tazama zote

Habari za hivi punde

  • WITO WATOLEWA KWA WATOTO WA KIKE KUPENDA MASOMO YA SAYANSI

    May 17, 2025
  • MAFIA KUUNGANISHWA NA UMEME WA GRIDI YA TAIFA

    May 16, 2025
  • WANANCHI WAASWA KUJITOKEZA KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 16, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI LARIDHIA KUANZISHWA KWA MRADI WA UONGEZAJI THAMANI ZAO LA DAGAA

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

MWENGE WA UHURU WAPONGEZA VIWANGO VYA BARABARA YA MSUFINI
Tazama Video zaidi

Viungo vya haraka

  • Home
  • Photo Gallery
  • FAQ
  • Tourism
  • Investment
  • MATOKEO YA STD VII 2022

Viungo vinavyohusiana

  • OR- TAMISEMI
  • OR- Menejimenti Utumishi wa Umma
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Pwani
  • Sekretarieti ya ajira katika Utumishi wa Umma
  • Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi
  • Wizara ya Fedha na Mipango

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Free Visitor&Stat Counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kilindoni-Bomani Street

    Anuani ya posta: 85

    Simu: 0232010199

    Simu ya mkononi:

    Baruapepe: ded.mafia@pwani.go.tz / ded@mafiadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Katazo
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma namba 1
    • YOUTUBE

Copyright ©2017 Mafia District Council . All rights reserved.