Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mafia Ndugu Salum Maulid leo Mei 31, 2025 amewaongoza watumishi, vikundi mbalimbali vya jamii pamoja na wananchi katika zoezi la usafi wa mazingira ikiwa zimebaki siku chache kuelekea Siku ya Mazingira Duniani inayoadhimishwa Juni 5, kila mwaka.
Akizungumza mara baada ya zoezi la usafi, na upandaji wa miti, Ndugu Maulid ameendelea kutoa wito kwa jamii kufanya usafi katika maeneo yao mara kwa mara bila kusubiri jumamosi ya mwisho wa mwezi.
Aidha, ametoa wito kwa jamii kutunza mazingira kwa kupanda miti kwa wingi na kuitunza ili kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.
Miti 143 imepandwa katika eneo la uwanja wa Mangosongo ( Mangosongo Arena) pamoja na kuokota plastiki pembezoni mwa barabara, ambapo tani 1.24 za plastiki zimeokotwa kuanzia uwanja wa Mangosongo mpaka eneo la Kigamboni, kwa Mpeta.
Kauli mbiu ya maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani kwa mwaka 2025 ni " Mazingira Yetu na Tanzania Ijayo, Tuwajibike Sasa; Dhibiti Matumizi ya Plastiki".
Kilindoni-Bomani Street
Anuani ya posta: 85
Simu: 0232010199
Simu ya mkononi:
Baruapepe: ded.mafia@pwani.go.tz / ded@mafiadc.go.tz
Copyright ©2017 Mafia District Council . All rights reserved.