• Wasiliana nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mafia District Council
Mafia District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais , Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mafia

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Ardhi, Mipango miji na Maliasili
      • Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
        • Kitengo cha Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Kilimo na Ushirika
      • Ujenzi na Zima Mmoto
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango na Takwimu
    • Vitengo
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ufugaji Nyuki
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Tehama
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
      • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Huduma za jamii
      • Maadili
      • Fedha, Utawala, na Mipango
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Kujua Sheria
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za Ofisi au Kitaifa
      • YOUTUBE
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

WAVUVI NA WAMILIKI WA VYOMBO WAASWA KUZINGATIA SHERIA KUEPUKA MIGOGORO NA SERIKALI

Posted on: October 17th, 2025

Mkuu wa Wilaya ya Mafia Mhe. Aziza Mangosongo amekitaka kikosi kazi kuhakikisha kuwa kinamaliza tatizo la uvuvi haramu kwa kuimarisha ulinzi baharini ikiwemo kufanya doria na kuwachukulia hatua za kisheria wahusika.

Mhe. Mangosongo ametoa agizo hilo leo Oktoba 17, 2025 wakati wa kikao chake na manahodha, wamiliki wa vyombo, wavuvi pamoja na viongozi wa BMU wilayani Mafia ambapo ameeleza nia ya Serikali katika kukomesha vitendo vya uvuvi haramu ambavyo vimekuwa vikipotosha mapato pamoja na kuharibu rasilimali.

Kwa upande wake, Afisa Uvuvi wa Wilaya Ndugu Alfahad Mohamed ametoa wito kwa wamiliki wa vyombo, manahodha na wavuvi kuzingatia sheria katika kazi zao ili kuepuka migogoro kati yao na Serikali pamoja na kuhakikisha kuwa wilaya inakuwa na rasilimali endelevu.

Wavuvi pamoja na viongozi wa BMU wameiomba Serikali kuwasaidia kwa kuwajengea uwezo zaidi ili waweze kutekeleza majukumu yao kwa ubora ikiwemo kusaidia katika kutokomeza uvuvi haramu pamoja na masuala ya uhifadhi wa rasilimali zilizopo kwa kuimarisha ulinzi katika maeneo yao.

"Tunashukuru kwa nafasi hii kukutana na kujadili, sisi changamoto tunayoipata katika shughuli yetu ni uvuvi haramu ambao mara nyingi unafanyika usiku, hivyo tunaomba tuimarishiwe ulinzi kwa kupatiwa vifaa ikiwemo kamera za kutusaidia kuwafuatilia pamoja na machine kwa ajili ya boti yetu ya doria" alieleza Bakari Mgaza, Mwenyekiti wa BMU kijiji cha Jojo.

Katika hatua nyingine ya kukomesha vitendo viovu wilayani Mafia, Mhe. Mangosongo ametoa wito kwa wavuvi kwa nafasi zao kuhakikisha kuwa wanakuwa mstari wa mbele katika kukemea vitendo ambavyo ni kinyume na maadili ikiwemo matumizi ya dawa za kulevya, ulevi uliokithiri pamoja na zinaa huku akitilia mkazo kutokujihusisha na wanawake wanaojiuza maarufu kama ' vijoti ' ambao wameenea kwa wingi katika maeneo mbalimbali.

Mhe. Mangosongo ameeleza kuwa ni muhimu kuzingatia sheria ndogo zilizopo wilayani ikiwemo zinazohusu mavazi katika jamii pamoja na kuwataka wamiliki wa sehemu za starehe kuzingatia sheria kama vile kufanya biashara zilizolengwa kutokana na vibali vyao bila kuruhusu biashara zisizofaa ambazo zimekuwa zikichangia kuleta mambo ambayo ni kinyume na maadili.


Matangazo

  • MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO; WASIMAMIZI WASAIDIZI NA MAKARANI (UCHAGUZI MKUU, 2025) October 20, 2025
  • Tazama zote

Habari za hivi punde

  • WAVUVI NA WAMILIKI WA VYOMBO WAASWA KUZINGATIA SHERIA KUEPUKA MIGOGORO NA SERIKALI

    October 17, 2025
  • MAFIA YAADHIMISHA JUMA LA ELIMU YA WATU WAZIMA

    October 09, 2025
  • UGAWAJI WA VYANDARUA WAZINDULIWA WILAYANI MAFIA

    October 08, 2025
  • SERIKALI YASISITIZA USHINDANI SOKO LA MWANI MAFIA

    October 06, 2025
  • Tazama zote

Video

USIKOSE KUWA SEHEMU YA TUKIO HILI MUHIMU KIHISTORIA
Tazama Video zaidi

Viungo vya haraka

  • Home
  • Photo Gallery
  • FAQ
  • Tourism
  • Investment
  • MATOKEO YA STD VII 2022

Viungo vinavyohusiana

  • OR- TAMISEMI
  • OR- Menejimenti Utumishi wa Umma
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Pwani
  • Sekretarieti ya ajira katika Utumishi wa Umma
  • Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi
  • Wizara ya Fedha na Mipango

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Free Visitor&Stat Counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kilindoni-Bomani Street

    Anuani ya posta: 85

    Simu: 0232010199

    Simu ya mkononi:

    Baruapepe: ded.mafia@pwani.go.tz / ded@mafiadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Katazo
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma namba 1
    • YOUTUBE

Copyright ©2017 Mafia District Council . All rights reserved.