• Wasiliana nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mafia District Council
Mafia District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais , Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mafia

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Ardhi, Mipango miji na Maliasili
      • Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
        • Kitengo cha Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Kilimo na Ushirika
      • Ujenzi na Zima Mmoto
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango na Takwimu
    • Vitengo
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ufugaji Nyuki
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Tehama
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
      • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Huduma za jamii
      • Maadili
      • Fedha, Utawala, na Mipango
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Inayoendelea
    • Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Taarifa
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Kujua Sheria
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za Ofisi au Kitaifa
      • YOUTUBE
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

WITO WATOLEWA KWA WATOTO WA KIKE KUPENDA MASOMO YA SAYANSI

Posted on: May 17th, 2025

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia na Mbunge wa Mafia Mhe. Omar Kipanga ametoa rai kwa wadau wote wa elimu wakiwemo viongozi na walimu kutoa ushirikiano kwa Serikali na wataalam mbalimbali ili kuhakikisha jamii inahamasisha watoto wa kike kupenda masomo ya sayansi.

Mhe. Kipanga ametoa rai hiyo leo Mei 17, 2025 wakati wa ufunguzi wa mradi wa uhamasishaji wa wanafunzi wa kike kupenda masomo ya Sayansi, Teknolojia, Uhandisi na Hesabu ( STEM) utakaotekelezwa na Tume ya Taifa ya UNESCO (Natcom) kwa kufadhiliwa na UNESCO.

" Mradi huu umekuja wakati mwafaka, wote tunazifahamu na kuendelea kuzifuatilia jitihada zinazofanywa na Serikali yetu ya Awamu ya Sita, hivyo naomba tutoe ushirikiano kwa wataalam wetu kuhakikisha jamii inahamasisha watoto wa kike kupenda masomo ya STEM" alisema Mhe. Kipanga.

Kwa upande wake, Mkuu wa Kitengo cha Sayansi Asilia kutoka Tume ya Taifa ya UNESCO Dkt. Joel Samuel ambaye amemuwakilisha Katibu Mtendaji wa Tume hiyo, amesema kuwa Tume kupitia mradi huu itafanyia kazi pia changamoto ya walimu wa sayansi ili kuhakikisha mradi huu unakuwa endelevu na kusaidia wanafunzi wa kike kupenda na kufanya vizuri katika masomo ya Sayansi , Teknolojia, Uhandisi na Hesabu.

Baadhi ya wazazi walioshiriki ufunguzi wa mradi huo wameahidi kushirikiana na walimu kuwahamasisha watoto wa kike wapende masomo ya sayansi ambayo mara nyingi wamekuwa wakiyaogopa

" Mimi nitakuwa balozi kwa kupita kila shule katika kata yangu kuongea na wanafunzi ili waweze kuyapenda masomo ya sayansi , pia nitahamasisha wazazi wenzangu kuwatia moyo watoto wa kike wapende masomo ya sayansi" ameeleza Mwajuma Ibrahim, Katibu wa Jumuiya ya Wazazi kata ya Kiegeani na mjumbe wa bodi ya shule ya sekondari Kitomondo.

Idadi ya wanafunzi wanaojiunga na mchepuo wa sayansi kwa sekondari imeongezeka kutoka 21 mwaka 2020 hadi kufika 55 mwaka 2023, hata hivyo, wanafunzi wa kike wanaojiunga na mchepuo wa sayansi ni wachache kulinganisha na idadi ya wanafunzi wa kiume ambapo ufaulu pia ni mzuri kwa wanafunzi wa kiume kuliko wa kike.

" Natamani tuendelee kupiga kampeni kuhakikisha watoto wa kike wanafikia ndoto zao bila kukatishwa kwa sababu kadhaa ikiwemo ujauzito, tukiwasimamia vizuri tutafanikiwa kupata wanafunzi wa kike wa masomo ya sayansi" alisema Bi. Khadija Mohamed, mwalimu wa somo la Baiolojia kutoka shule ya sekondari Kitomondo.

" Walimu ni watu wa kwanza wa kufanya watoto wa kike wapende masomo ya sayansi, hivyo tutengeneze urafiki kwa watoto wetu wa kike ili wapende masomo ya sayansi". Kwa upande wangu, mwaka 2024 kwa kidato cha nne, wanafunzi 100 walifaulu somo la Baiolojia na kulikuwa na alama 'A' moja ambayo aliipata mtoto wa kike, na alama B za kutosha pamoja na alama C . Alieleza.

Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozaji wa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imefanya jitihada nyingi kuhakikisha mtoto wa kike anapata elimu bora, miongoni mwa Juhudi hizo ni pamoja na ujenzi wa shule maalum 26 za sayansi za wasichana katika mikoa, ujenzi wa bweni kwa wanafunzi wa kike kuwapunguzia umbali waendapo shule, utungaji na utekelezaji wa sheria na miongozo mbalimbali inayotoa fursa kwa wanafunzi wa kike kutimiza ndoto zao, wanafunzi wanawake kupewa kipaumbele katika programu mbalimbali kama vile ufadhili wa masomo " Samia Scholarship" na kuimarisha mifumo ya utawala bora.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUONGEZWA MUDA WA KULIPIA VIWANJA May 20, 2025
  • Tazama zote

Habari za hivi punde

  • WITO WATOLEWA KWA WATOTO WA KIKE KUPENDA MASOMO YA SAYANSI

    May 17, 2025
  • MAFIA KUUNGANISHWA NA UMEME WA GRIDI YA TAIFA

    May 16, 2025
  • WANANCHI WAASWA KUJITOKEZA KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 16, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI LARIDHIA KUANZISHWA KWA MRADI WA UONGEZAJI THAMANI ZAO LA DAGAA

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

MWENGE WA UHURU WAPONGEZA VIWANGO VYA BARABARA YA MSUFINI
Tazama Video zaidi

Viungo vya haraka

  • Home
  • Photo Gallery
  • FAQ
  • Tourism
  • Investment
  • MATOKEO YA STD VII 2022

Viungo vinavyohusiana

  • OR- TAMISEMI
  • OR- Menejimenti Utumishi wa Umma
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Pwani
  • Sekretarieti ya ajira katika Utumishi wa Umma
  • Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi
  • Wizara ya Fedha na Mipango

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Free Visitor&Stat Counter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Kilindoni-Bomani Street

    Anuani ya posta: 85

    Simu: 0232010199

    Simu ya mkononi:

    Baruapepe: ded.mafia@pwani.go.tz / ded@mafiadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Katazo
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma namba 1
    • YOUTUBE

Copyright ©2017 Mafia District Council . All rights reserved.